KAMISHNA wa Skauti Mkoa wa Shinyanga,Mussa Chama akiongea. |
CHANGAMOTO kubwa
inayosababisha hamasa ya Skauti kupungua,ni kutokana na Serikali za wilaya
kutotoa kipaumbele
kwa watenda kazi wa vikundi vya skauti kwa kuhakikisha wanawatengea bajeti,sambamba na wazazi kuwazuia vijana wao kwa madai huteswa kwa kupewa adhabu mbalimbali.
kwa watenda kazi wa vikundi vya skauti kwa kuhakikisha wanawatengea bajeti,sambamba na wazazi kuwazuia vijana wao kwa madai huteswa kwa kupewa adhabu mbalimbali.
MZAZI Chacha Marwa akitoa neno. |
Hayo
yalielezwa na Kamishna wa Skauti Mkoa wa Shinyanga,Mussa Chama,wakati wa
uzinduzi wa Klabu ya Mazoezi ya Skauti wilayani Kahama,ambapo hakusita kueleza
jinsi serikali ilivyowatelekeza watendaji kazi wa Skauti kwa kushindwa kuwapangia
bajeti huku wakitambua umuhimu wa kambi za Skauti.
VIJANA wa Skauti wakiimba kwa pamoja. |
Alisema
kuwepo kwa skauti kunasaidia kutoa mafunzo ya uzalendo kwa vijana,hivyo
kuwajengea maadili mema ya Kitanzania na kuwaepusha kujiunga na vikundi
visivyofaa ambavyo vimekuwa kichocheo cha vijana wengi kujitumbukiza katika
matumizi ya madawa ya kulevya.
VIJANA wa Skauti wakiimba. |
Kamishina
huyo wa skauti,alisema wamekuwa wakifanya kazi hiyo kwa mazingira magumu
kutokana na kutokuwa na mafungu ya kuwaweka mara kwa mara kambini vijana ili
kuwapatia stadi za kazi na kuwajengea uzalendo wa taifa vijana.
VIJANA wa Skauti wakicheza muziki. |
“Skauti
imesahaulika wakati ndio kichocheo kikubwa cha vijana kuepuka matumizi ya
madawa ya kulevya,kwa kupatiwa mafunzo yenye maadili mema,na mioyo ya kujitolea
katika shughuli mbalimbali ili kujenga uzalendo wa Taifa letu,”Alisema
Kamishina Chama.
VIJANA wa Skauti wa Kike wakicheza. |
Aidha
alisema kulikuwa na umuhimu wa Serikali kuzielekeza Halmashauri kupanga bajeti
kwa ajili ya Skauti,hali itakayowarahisishia watendaji wake kuwaweka mara kwa
mara vijana kambini na kuwajengea uzalendo wa kulipenda taifa.
MABINTI wakionyesha umahiri wa kucheza muziki. |
Hata
hivyo Chama alisema mbali na serikali kuwasahau wamekuwa wakitafuta ufadhili
kwa wafanyabiashara ili kuwaweka vijana kambini,lakini wamekuwa wakipata
vikwazo kwa baadhi ya wazazi ama walezi ambao wamekuwa na hisia tofauti na
masuala ya Skauti.
FARAJA Isack,akisoma risala. |
Alisema
wazazi na walezi wamekuwa wakizuia vijana wao kujiunga na kambi za skauti kwa
imani kuwa watakumbana na mateso kutokana na adhabu wanazopatiwa pasipo
kutambua lengo la kambi hizo ni kuwajengea vijana ukakamavu sambamba na kuwajengea nidhamu
njema.
BAADHI ya wazazi na walezi waliohudhuria uzinduzi. |
“Maisha
ya skauti yanatawaliwa na uzingatiaji wa nidhamu,pamoja na stadi zinazowajenga
vijana kuishi katika mazingira yoyote yale huku wakiwa na mioyo ya kizalendo
kwa Taifa na si vinginevyo,”Alisema Chama.
MAMA Simba akijiandaa kufungua shampeni ya Uzinduzi. |
Kwa upande wake Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa
Kahama,Felix Kimario,aliwapongeza Skauti
kutokana na kuwa mstari wa mbele katika shughuli mbalimbali za kujitolea
katika jamii.
Alisema
kambi za Skauti ni muhimu kuendelea kuwepo kwa ajili ya kukabiliana na
mmomonyoko wa maadili kwa vijana,kwa
kuwaweka vijana pamoja kubadilishana
mawazo na kelekezana maadili ya Kitanzania,hivyo kuwaasa wazazi kuwahamasisha
vijana wao kujiunga na Skauti.
MKURUGENZI Mtendaji wa Halmashauri ya Mji wa Kahama,Felix Kimario,akimkabidhi kadi ya uanachama wa Skauti kijana.
Nae
mzazi Chacha Marwa,aliwashangaa wazazi ambao wamekuwa wakilalamika juu ya
vijana wao kutokuwa na maadili na utamaduni wa Kitanzania,huku walishindwa
kuwahamasisha na kuwasimamia kujiunga na Skauti ili kupatiwa mafunzo ambayo
yangejenga uzalendo na maadili mema kwa vijana wao.
Skauti
wilaya ya Kahama imefungua Klabu ya mazoezi mbalimbali ya mwili,ambayo lengo
lake na kuwafanya vijana na watu wa rika mbalimbali kushiriki mazoezi hayo ili
kujenga afya zao,na kuwaondoa vijana katika makundi hatarishi ambayo yanaweza
kuwasababisha kutumia madawa ya kulevya.
|