WAKIKAGUA Maktaba. |
Hayo yalielezwa na Mkuu wa
Shule hiyo,Melkisedeck Choya,alipokuwa akisoma risala katika uzinduzi wa
maktaba ya shule hiyo,ambapo alikiri kwa kipindi kirefu ufanisi wa kitaaluma
shuleni hapo unakabiliwa na kukosekana kwa umeme sambamba na kutokuwepo kwa
maabara.
KWAYA ya Shule ikitumbuiza katika hafla hiyo fupi. |
Choya alisema pamoja na
kuwezeshwa kuwa sekondari ya kwana katika Halmashauri ya Mji wa Kahama,kuwa na
Maktaba itakayosaidia kuongeza taaluma kwa wanafunzi kwa kwenda kujisomea na
kuazima vitabu vya kiada na ziada,lakini ukosefu wa miundo mbinu ya umeme
utaendelea kuathiri ufanisi katika shule hiyo.
Alisema mbali na miundo
mbinu ya Umeme,pia upungufu wa viwanja vya michezo katika shule hiyo kunaathiri
kuibua vipaji vya vijana katika sekta hiyo ambayo katika karne hii inazalisha
ajira,huku akisema kuwepo kwa maktaba hiyo kutaongeza ufaulu kwa vijana shuleni
hapo.
MENEJA wa Atlas Copco,Tawi la Mwanza,Menas Ngonyani akizungumza na wanafunzi . |
“Kwa kipindi kirefu tangu
kuanzishwa kwa shule hii hatukuwa na Maktaba,jambo liliofanya walimu wafanye
kazi ya ziada ili kuhahakisha wanafunzi wanafyanya vizuri katika mitihani
yao,lakini sasa tumerahisishiwa kuwepo kwa maktaba hii,tutaitumia vizuri walimu
pia wanafunzi ili kuhakikisha shuleni yetu inafanya vyema katika mitihani ya
taifa,”Alisema Choya.
IGIZO la Wanafunzi. |
Kwa upande wake Meneja wa
Atlas Copco,Tawi la Mwanza,Menas Ngonyani,alisema kampuni yake ambayo inafanya
kazi katika Kanda ya ziwa tangu mwaka 2008,imeona irejeshe pato wanalozalisha
kwa kusaidia huduma za jamii katika sekta mbalimbali.
MWANAFUNZI wa Kidato cha Kwanza katika Shule ya Sekondari ya Kishimba,Fatma Miraji,akifurahia zawadi yake. |
Aidha aliwaomba walimu
katika shule hiyo kuitumia maktaba hiyo kwa kuanzisha timu za masomo mbalimbali
kwa wanafunzi ili kuleta ushindani wa kitaaluma utakaosaidia kufanya vyema kwa
wanafunzi katika shule hiyo.
BAADHI ya Wanafunzi wakiwa Maktaba. |
MWALIMU Prosper Donard,akielekeza wanafunzi. |
“Msihadaike na wanaosoma shule
za English Medium,Yes …No ni ileile,cha msingi muwe makini katika kuwasikiliza
walimu wenu na kuzingatia maadili ya uanafunzi na shule,mtafanya vyema kuliko
hata waliopelekwa hizo shule za Pesa,”Alisema Asha.
MKUU wa Shule ya Sekondari ya Kishimba,Melkisedeck Ngonyani,akisoma Risala. |
Maktaba katika shule hiyo
imekarabatiwa na Shirika la Read International chini ya ufadhili wa Atlas
Copco,na kugharimu kiasi cha Shilingi Milioni Nane,kwa kuhusisha upakaji
rangi,kutengeneza kabati za kuhifadhi vitabu,meza na viti sambamba na vitabu
vya kiada na ziada.