Sunday, July 26, 2015

LEMBELI ATIKISA KAHAMA *ABEBWA KAMA MFALME KATIKA MAPOKEZI YAKE *UMATI MKUBWA WA WATU WAMTOA MACHOZI

BOFYA HAPA CHINI KUONA MAAJABU YA LEO

JAMES Lembeli akibebwa kama Mfalme.


ALIYEKUWA Mbunge wa  Jimbo la Kahama,James Lembeli,kupitia Chama cha Mapinduzi “CCM” ambaye hivi karibuni ametangaza kukihama chama hicho na kujiunga na Chama cha Demokrasia na Maendeleo,jana alipokelewa na umati mkubwa wa watu
Mjini Kahama huku akibebwa Kifalme.



BODABODA  katika mapokezi ya Lembeli.


Mapokezi hayo ambayo hayajapata kutokea kufanyika kwa kiongozi wa aina yeyote wilayani Kahama,yalianzia mji mdogo wa Tinde kilometa zipatazo 38 kutoka mji wa Kahama na kuingia mjini majira ya saa 9:30,yaliongozwa na bodaboda zaidi ya 100,bajaji na magari yalisimamisha shughuli za kiuchumi katika mji wa Kahama kwa masaa matatu.

BODABODA wakiongoza msafara wa mapokezi ya Lembeli.


Katika msafara huo wananchi hao walifunga barabara zote za mji wa Kahama hali iliyosababisha magari kusimama kuunga foleni ndefu mpaka walipofika kwenye viwanja vya CDT ambapo mkutano huo mkubwa ulifanyika,ukiongozwa na Wabunge waliomaliza muda wao wa Majimbo ya mkoani Mwanza,Highness Kiwia na Ezekia Wenje sambamba na Mbunge wa Biharamulo,Athony Mbassa.

JAMES Lembeli alipokuwa akiingia mjini Kahama.


Wakiwa katika mkutano huo Katibu wa Chadema Mkoa wa Shinyanga, Zacharia Thomas,alimwelezea Lembeli kuwa ni  mwanasiasa aliyekomaa,mpenda haki lakini kuwepo kwake CCM,kulikuwa sawa na kuifukia nyota yake jalalani ambapo itang’ara maradufu baada ya kujiunga CHADEMA.


WATU wenye miraba minne wakimbeba Kifalme Lembeli.


Akiongea katika mkutano wa hadhara,mbunge wa Jimbo la Ilemela,Kiwia aliwataka wananchi wa Kahama pamoja na kumuunga mkono Lembeli, wanapaswa kuwa na nguvu ya pamoja pindi akipita katika kura za maoni za CHADEMA kwa kuhakikisha wanapiga na kulinda kura ili kudhibiti wizi wa kura ambao unawezwa kufanywa na wasimamizi wa uchaguzi.


UMATI wa watu uliohudhuria mapokezi ya James Lembeli.


Alisema Lembeli anaweza kushinda kwa kura nyingi katika Jimbo la Kahama mjini, lakini anaweza kuhujumiwa na wasimamizi wa uchaguzi ambao ni Wakurugenzi wa halmashauri hali ambayo alisema wasimamie kwa nguvu ushindi wake.

JAMES Lembeli katika muonekano wa CHADEMA


Kwa upande wake Lembeli aliyekuwa ameambatana na mama yake Mzazi, Maria Kasembo, alisema uamuzi alioufanya ulikuwa ni mgumu lakini wizi na rushwa iliyokuwa ikifanyika katika ofisi za CCM ilimlazimu kuamua uamuzi mgumu wa kuhama na kujiunga na CHADEMA.

UMATI wa watu katika Mkutano wa Hadhara



Lembeli ambaye alikuwa akihutubia umati mkubwa  wa wananchi kwa kutumia kitabu cha Biblia alisema uamuzi wake huo ni sawa na Mwana aliyekuwa amepotea na sasa amerudi kuwakomboa wana wa Israel.
JAMES Lembeli akianza hotuba kwa kusoma Biblia.


Alisema kuhama kwake CCM na kwenda chadema atafanya kazi kubwa ya kutetea wanyonge kuliko alivyokuwa akitetea akiwa ndani ya CCM sehemu iliyojaa wizi na rushwa.

JAMES Lembeli akifuta chozi lililombubujika ghafla.





Hata hivyo alipofikia kueleza kilichomtoa CCM Lembeli aliangua kilio akisema pamoja na kufanya kazi kubwa hakupewa shukurani badala yake akawa mtu wa kuletewa wala rushwa na watoa rushwa ili wagombee ubunge kwenye jimbo lake la Kahama.

LEMBELI akiongea na umati wa watu katika viwanja vya CDT


Aidha alisema CCM imenuka rushwa hasa katika ngazi ya Wilaya ili uweze kukubalika kugombea ni lazima utoe rushwa kwa viongozi wa juu wa CCM Wilaya hali ambayo alipingana nayo na kuonekana ni msaliti ndani ya chama.

LEMBELI akifafanua jambo



Pia alisema pamoja na kugombea ubunge jimbo la Kahama Mjini kama atashinda na kuwa mbunge atasaidia wananchi wote wa Majimbo ya Kahama na Ushetu jimbo ambalo limezaliwa kutoka Kahama ambayo kwa pamoja ameyatumikia kwa miaka 9 na nusu anajua matatizo ya wananchi wote wa majimbo hayo

Nae mbunge wa jimbo la Nyamagana aliyemaliza muda wake Wenje alisema anamtambua Lembeli hata alipokuwa mbungeni misimamo yake ilionyesha kama mpinzani hivyo kuhama kwake CCM huko alikokuja ndiko atakavyofanya kazi vizuri

SEHEMU ya umati uliomlaki Lembeli.



Wenje alisema Chadema hakuna mgeni mwanachama yeyote akiingia leo anaanza kazi  hapo hapo hivyo Lembeli tangu siki aliyoingia alianza kazi siku hiyo na ndiyo maana alikwenda Bunda kufanya kazi za chama hivyo Kahama wamuunge mkono.
                                                                      

 
ya kadamnasi.  
 
 
Kwa kutumia mkutano huo Lembeli alitangaza rasmi kuwania ubunge jimbo la Kahama mji na kuwatoa wasiwasi wagombea wengine wa chama chake kipya kuwa demokrasia itazingatiwa wakati wa mchakato wa kura za maoni ndani ya chama ili kupata mgombea stahiki na atakuwa tayari kumuunga mkono kada yeyote wa Chama hicho atakayeteuliwa kupeperusha bendera ya CHADEMA.

KUONA VIDEO MPYA BOFYA HAPA CHINI