Wednesday, July 15, 2015

"JINSI SI KIGEZO CHA KUTOKUWA MWAKILISHI WA WANANCHI"SHDEPHA+

BOFYA HAPA CHINI KUONA MAAJABU YA LEO

MKURUGENZI wa Shdepha+,wilayani Kahama,Venance Mzuka.
WAKATI Taifa likielekea katika Uchaguzi Mkuu,jamii imetakiwa kuchagua viongozi kutokana na uwezo na si
kuangalia jinsi,sambamba na wanawake kushauriwa kujitokeza kuwania nafasi za kuchaguliwa ili wawakilishe wananchi kwa kujiamini.
MJUMBE katika Mdahalo,Mama Baranoga.

Mwito huo ulitolewa na Mkurugenzi wa Miradi Shdepha+,Kanda ya Ziwa,Venance Mzuka,katika Mdahalo wa siku moja uliohusisha vikundi vya Wajasiriamali wa Kata ya Nyasubi katika Halmashauri ya Mji wa Kahama,ambapo aliwahamasisha wanawake kujitokeza kuwania Ubunge na Udiwani.

MWEZESHAJI katika Mdahalo huo,Rajab Thomas.
Mzuka aliviomba vyama vya siasa kutoa kipaumbele kwa wanawake ambao wataonyesha nia ya kutaka kuwakilisha wananchi katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 25,mwaka huu ilimradi wawe wamekidhi vigezo vya kuwa wagombea sahihi.
MSHIRIKI katika Mdahalo;Munge Kuhoka kutoka Kahama Artistic and Entertaiment Group.
Nae Afisa Miradi wa Shdepha+ wilayani Kahama,Rajab Thomas,aliwaomba wanawake waondokane na hofu ya mfumo dume ya kujiona stahili yao ni kuchagua wawikilishi kwa kupiga kura huku wakisubiri uteuzi wa viti maalumu.
MWEZESHAJI Rajab Thomas,akiongea na washiriki wa Mdahalo.
Thomas alisema Shirika lake linatekeleza Mradi wa Fahamu,Ongea na Sikilizwa ambao unaratibiwa na Shirika la OXFAM Tanzania baada ya Kupata ufadhili kutoka OXFAM Ireand wenye lengo la kuwahamasisha na kuwatia ujasiri wanawake watambue haki ya kujiandikisha,kupiga kura na kuchaguliwa.
MSHIRIKI katika Mdahalo;Samson Kabiligi.


Hata hivyo Thomas alisema japokuwa mradi umelenga zaidi wanawake lakini abadani hauwezi kufanikiwa pasipo kumhusisha mwanaume,ambaye katika kuelekea kipindi hiki cha uchaguzi anawajibu mkubwa wa kumtia ujasiri mwanamke ili ashiriki kikamilifu katika uchaguzi.


WASHIRIKI wa Mdahalo katika mjadala wa Vikundi.
Alisema wanawake wasijione duni bali watambue wanawajibu wa kushiriki kikamilifu katika uchaguzi wa mwaka huu kwa kujitokeza kwa wingi kuwania Ubunge na Udiwani na kuondokana na kawaida yao ya kusubiri kudra ya viti maalum.

Aidha aliwaomba wananchi wawapime wanawake watakoajitokeza kwa vigezo na si kwa jinsi,kusudi wamudu kuingia katika vikao vya maamuzi na kutetea stahiki zao na za jamii kwa ujumla,huku akiwataka wanawake kutokatishana tamaa pindi miongoni mwao atajitokeza kuwania Udiwani ama Ubunge.
MMOJA wa Maafisa wa SHDEPHA +
Mmoja wa Washiriki hao,Mwalimu Luhumbika Japani,alitia shaka kujitokeza kwa wingi wanawake katika nafasi za Ubunge na Udiwani,kutokana na kutokuwepo kwa elimu ya Uraia inayostahili kwa jamii kuona umuhimu wa zoezi la kujiandikisha,kupiga kura na kujitokeza kuwania uongozi.
WASHIRIKI wa Mdahalo.
WASHIRIKI wa Mdahalo wakijaza fomu.

KAIMU Afisa Mtendaji kata ya Nyasubi akihitimisha Mdahalo.


Shinyanga,Shinyanga Vijijini na Kahama mji ili kuwajengea uelewa kwa jamii katika muktadha mzima umuhimu wa kujiandikisha,kupiga kura na kuchagua ama kuchaguliwa uli kuleta usawa wa jinsi katika vikao vya maamuzi.

















Mwalimu Japani alisema uduni wa elimu ya uraia inaweza kuchangia kutokuwepo kwa mwamko mkubwa wa wanawake kujitokeza kuwania nafasi hizo za uwakilishi sambamba na kupiga kura.

 SHDEPHA+ inatekeleza mradi huo katika Halmashauri za Manispaa ya

KUONA VIDEO MPYA BOFYA HAPA CHINI