Wednesday, July 22, 2015

ISAKA KUMEKUCHA KINYANG'ANYIRO CHA UDIWANI TIKETI YA CCM

BOFYA HAPA CHINI KUONA MAAJABU YA LEO

NDUGU Gerald Mwanzia,akikabidhiwa Fomu na Katibu wa CCM,Kata ya Isaka,Mathias Ndabila.
 
MAKADA watano wa CCM katika Kata ya Isaka wamejitokeza kuwania kuchaguliwa na chama hicho kupeperusha bendera ya chama hicho katika nafasi ya Udiwani akiwemo Diwani
aliyeiongoza Kata hiyo kwa mwaka 2005 hadi 2010.

Dr.Gerald Mwanzia akionyesha Fomu alizochukua za Udiwani.
Kada huyo wa CCM,mwenye taaluma ya Daktari wa binadamu,Dk.Gerald Mwanzia,alichukua fomu hiyo na kukamilisha idadi hiyo ya makada watano,huku akisema iwapo atapata ridhaa ya kuongoza Kata hiyo atahakikisha anaboresha sekta zote zilizozorota kipindi akiwa hayupo madarakani.

Dk.Mwanzia alisema kuwa kipindi akiongoza Kata hiyo,alifanikisha kukamilisha ujenzi wa maabara ya sayansi katika Shule ya Sekondari ya Kata hiyo,kabla hata ya agizo la Rais wa Jamhuri ya Muungano alilotoa kuwepo kwa maabara hizo kwa kila sekondari za serikali nchini.
MTANGAZAJI wa Baloha FM,Ndalike Sonda,akifanya mahojiano na Dr.Mwanzia.
Alisema kipindi akiongoza Kata hiyo maendeleo katika sekta za Elimu,Afya na Maji sambamba na uchumi wa wakazi wa kata hiyo vilikuwa vinachukua kasi tofauti na hali ilivyo kipindi hiki hali iliyomfanya awanie nafasi hiyo tena kusudi ashirikiane na wananchi wa kata hiyo kufikia maendeleo yanayostahili.

Mbali na Dk,Mwanzia ambaye alichukua fomu na kuirejesha,wengine waliochukua na kurejesha ni pamoja na mwanajeshi mstaafu wa JWTZ,Pili Izengo,Mwanamichezo maarufu katika Kata hiyo,Pazi  Majuto Pazi,aliyekuwa Mwenyekiti wa Kijiji cha Bandari,Said Hamadi “Shantuti”na Justine Akuziwe.

KUONA VIDEO MPYA BOFYA HAPA CHINI