Friday, June 5, 2015

WANANCHI JITOKEZENI KESI ZA ALBINO

BOFYA HAPA CHINI KUONA MAAJABU YA LEO



 Na Jackson Bahemu,
Kahama.

WANANCHI wametakiwa kuacha kulalamikia ucheleweshaji wa hukumu za watuhumiwa wa mauaji ya Albino,badala yake wawe mstari wa mbele kutoa
ushahidi pindi matukio hayo yanapojitokeza,hatua itakayosaidia hukumu kutoka kwa wakati.

Rai hiyo ilitolewa na Afisa Mchunguzi Mkuu,toka Tume ya haki za Binadamu na utawala bora,makao makuu  Dar Es Salaam,Peter Massawe,wakati wa warsha  ya Siku Tatu ya kuandaa mkakati wa kutokomeza mauaji,ubaguzi na unyanyapaa kwa Albino.

Katika warsha hiyo,iliyoandaliwa na Shirika la Elimu,Sayansi na Utamaduni la Umoja wa Mataifa “UNESCO”,na kuwashirikisha wadau mbalimbali,ikiwa na lengo kuu la kushirikisha jamii kugundua chanzo cha tatizo la mauaji hayo ili kuyadhibiti.

Massawe alisema kuwa jamii nchini imekuwa hodari wa kulalamika pindi hukumu za watuhumiwa zinapochelewa ama kutolewa kwa kuwaachia huru,huku ikiwa nyuma katika suala la kujitokeza kutoa ushahidi wa kuwatia hatiani Watuhumiwa.

“Ili hukumu stahiki na zinazotarajiwa zipatikane,ni budi tuondoe hofu ya kusaidia polisi,japo inadaiwa wao ndio chanzo cha kutojitokeza kutoa ushahidi kutokana na usumbufu wao kwa anaejitokeza kusaidia Polisi,”Alisema Massawe.

Hata hivyo wadau hao waliitupia lawama serikali kuchelewesha utekelezaji wa hukumu za vifo zilitolewa kwa waliotiwa hatiani jambo ambalo limesababisha kuendelea kwa matukio hayo.

Afisa Mtendaji wa Kata ya Chela,Patrick Mahona,alisema mbali ya serikali kutotekeleza hukumu ya Mahakama ya kuwanyonga waliotiwa hatiani,ni kiini cha kuendelea kuibuka kwa vitendo hivyo vya kikatiri.

Aidha alisema hata mashirika ya haki za binadamu yanachangia kuendelea kuwepo kwa vitendo hivyo,kwakuwa yamekuwa mstari wa mbele kupinga adhabu ya vifo kwa wanaobainika na kudhiirika kwa makosa ya mauaji ya watu wenye ulemavu wa ngozi.

Akihitimisha warsha hiyo,Afisa Mratibu wa UNESCO,Mathias Herman,alisema lengo la warsha hiyo,ni kutafiti mbinu mbadala ya kutowapeleka makambini Albino,kitendo kinachoonyesha ni cha kibaguzi.

Herman alisema UNISCO imeona vyema kuwafikia wananchi,ili kupanga mkakati utakaonusuru jamii hiyo kuepukana na ubaguzi,unyanyasaji na mauaji hayo kuendelea ambapo wanatekeleza mradi huo katika wilaya nne za Kanda ya Ziwa.

KUONA VIDEO MPYA BOFYA HAPA CHINI