Thursday, April 16, 2015

WANAWAKE WATAKIWA KUJIKOMBOA KIUCHUMI ILI KUEPUKA UKATIRI WA KIJINSIA.

BOFYA HAPA CHINI KUONA MAAJABU YA LEO


 WANAWAKE nchini wametakiwa masuala yao kuwa endelevu na si kungoja na kuitumia siku ya Wanawake Duniani,kujitafakari katika suala la huruma na upendo sambamba
na kujiwekea malengo ya kujikomboa kiuchumi na kijamii ili kupunguza vitendo vya manyanyaso ikiwemo ukatili wa Kijinsia.

 
Kauli hiyo ilitolewa na Mwenyekiti wa Baraza la Wanawake la CHADEMA"BAWACHA",wilaya ya Msalala,Asha Binde, wakati alipojumuika na wanachama Baraza hilo,kutembelea wagonjwa waliolazwa katika Kituo cha Afya cha Lunguya kilicho Halmashauri ya Msalala wilayani Kahama,ambapo alisema kujikomboa kiuchumi kutawaondoa katika vitendo vya kunyanyaswa.
 
Binde alisema wanawake waondokane na dhana kuweza pasipo kuwezeshwa kila inapofika maadhimisho bali uwezesho huo uwe endelevu katika maisha ya kila siku,kwa kujituma katika shughuli mbalimbali za kijamii ili kuondokana na utegemezi,na nafsi zao zikitawaliwa na upendo,huruma kwa jamii zenye matatizo.
 
“Dhana ya wanawake kuweza bila kuwezeshwa iwe endelevu katika maisha yetu isingoje maadhimisho tu,tujitume katika kazi na tuwe na huruma na upendo kwa jamii inayoguswa na matatizo kila mara kwa kuwatembelea waagonjwa na kuwasaidia huduma mbalimbali mbali ya kuwapa pole,”Alisema Binde.
 
Aidha aliwaomba wanawake wajitokeze kujiandikisha katika daftari la kudumu la upigaji kura sambamba na kujitokeza kuwania nafasi za Udiwani na Ubunge katika Uchaguzi mkuu wa mwaka huu,ili kutumia fursa hiyo kama njia ya kupata haki zao zinazostahili.
 
Mwenyekiti huo wa Bawacha wilaya ya Msalala aliwaomba wanawake wafanye mabadiriko ya kifikra kwa kuondokana na mazoea ya kuchagua wawakilishi kwa kununuliwa bali yawe matakwa yao halisi kwa kiongozi wanayemhitaji.












 

 


 
 
 
 
 

KUONA VIDEO MPYA BOFYA HAPA CHINI