Tuesday, June 30, 2015

MAFAO HUWAACHISHA KAZI WATUMISHI MIGODINI

BOFYA HAPA CHINI KUONA MAAJABU YA LEO

NAIBU Waziri wa Nishati na Madini,Charles Kitwanga,mwenye suti akikabidhi mfano wa Hundi yenye thamani ya Shilingi Milioni Mia Tisa, kwa Meneja Ufanisi wa Kampuni ya Bulyanhulu - Acacia,Elias Kasitila,kwa ajili ya Buika SACCOSS.
Mifuko ya Kijamii ni kichocheo kikubwa cha watumishi hao kuacha kazi migodini.

Hayo yalibainishwa juzi na Mwenyekiti wa Buika SACCOS, Agapiti Kisoka, katika hafla fupi ya kukabidhiwa hundi ya shilingi milioni 900 kutoka katika Mfuko wa Pensheni wa PPF kwa lengo la kukuza mtaji  kwa Chama cha kuweka na kukopa kilichopo mgodini hapo.
WANACHAMA wa Buika SACCOSS

Kisoka alisema  asilimia kubwa ya wafanyakazi walio wengi walikuwa wakifanya kazi huku wakienda kuangalia mafao yao kila mwezi katika mifuko hiyo ya pensheni hali ambayo imechangia kwa kiasi kikubwa kupungua kwa wafanyakazi katika migodi hiyo pindi wanapoona wanakiasi kikubwa cha fedha walichochangia katika mifuko hiyo.
MENEJA wa PPF tawi la Kahama,James.


Alisema kutokana na hali ya mfuko huo wa PPF kwa kutoa fedha hiyo ili kuzidi kuiongezea mtaji Saccos ya Buika ambayo mpaka kufikia sasa ina wanachama 634 sawa na asilimia 30 ya watumishi wa mgodi huo,utasaidia kuendelea kuwapa nafuu ya maisha wanachama wake.

“Fedha hizi zilizotolewa na mfuko wa pensheni wa PPF zitatusaidia katika mambo mbalimbali yakiwamo ada za watoto pamoja na matatizo mbalimbali ya kijamii yanayotokea katika familia za wafanyakazi kwa mikopo ya papo kwa papo kwa kiwango kisichozidi milioni moja,”alisema mwenyekiti huo.
NAIBU Waziri wa Nishati na Madini,Charles Kitwanga na Meneja wa Mgodi wa dhahabu wa Bulyanhulu unaomilikiwa na Kampuni ya ACACIA,Michelle Ash,wakifurahia jambo.
Naye mwakilishi wa mkurugenzi wa PPF Selestine Some alisema kuwa Saccos nyingi zilizopo katika maeneo ya kazi zimekuwa mkombozi mkuwa kwa wafanya kazi na kuitaka mifuko mingine ya kijamii kujitokeza katika kutoa mikopo katika maeneo mbalimbali ya kazi.


Alisema mkopo uliotolewa kwa wafanyakazi hao utakuwa na kiwango cha riba nafuu  ya asilimia kumi na itatolewa kwa kipindi cha kuanzia miaka tatu hadi mitano na kuongeza kuwa sharti la kupata mkpo huo nikuwa mwanachama wa PPF.
MENEJA Ufanisi wa Kampuni ya dhahabu ya Bulyanhulu inayomilkiwa na ACACIA,Elias Kasitila anayeandika akiwa na Mwakilishi wa Mkurugenzi wa PPF,Selestine Some.
Some alisema katika kipindi cha miaka kumi iliyopita mfuko wa PPF nchini tayari umekwisha toa mikopo ya Zaidi ya shilingi Bilion 86.82 kwa saccos zilizopo katika maeneo ya kazi na kuongeza wengi walitumia mikpo hiyo kujiendeleza katika elimu na kukuza uchumi wao kupitia kilimo.
NAIBU Waziri Charles Kitwanga,akihotubia.

 
Kwa upande wake Naibu Waziri wa Nishati na Madini Charles Kitwanga alimuomba Meneja wa Mgodi huo Michelle Ash kuangalia uwezekano wa kuwaongeza fedha kwenye mfuko huo ili wafanyakazi wapate hamasa na kumudu kukopa kiasi kikubwa cha pesa ili kukidhi mahitaji yao.

 

 

 

 

 

 

 

 

 

KUONA VIDEO MPYA BOFYA HAPA CHINI