WITO
umetolewa kwa Viongozi wa Serikali ngazi ya kata kujenga mahusiano mazuri na jamii
inayowazunguka katika maeneo yanayozunguka Migodi ya Acacia Wilayani Kahama
Mkoani Shinyanga ili kuepusha
migogoro ya ardhi inayoweza kutokea na kusababisha uvunjifu wa amani.
Hayo yalisemwa jana na Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Msalala Elikana Masota katika Mafunzo ya Amani endelevu na ulinzi na usalama katika maeneo yanayozunguka migodi ya Acacia yaliondaliwa na Shirika lisilo la Kiserikali la Search For Common Ground La Mjini Kahama.
Katika mafunzo hayo yaliojumuisha yaliojumuisha viongozi mbalimbali kutoka katika kata zilizo jirani na Migodi ya Dhahabu ya Bulyanhulu pamoja na Buzwagi yallikuwa na lengo la kuelimisha viongozi hao juu ya Sera ya ardhi ili kutokuleta mifarakano na wawekezaji.
Alisema kuwa migogoro mbalimbali inayotokea imekuwa ikisababishwa na kutoshirikishwa kwa Wananchi katika kutatua matatizo mbalimbali yanayohusika na ardhi hali ambayo inasababisha mifakano baina ya Mwekezaji na mmiliki wa ardhi wakati malipo ya fidia
KUONA VIDEO MPYA BOFYA HAPA CHINI
migogoro ya ardhi inayoweza kutokea na kusababisha uvunjifu wa amani.
Hayo yalisemwa jana na Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Msalala Elikana Masota katika Mafunzo ya Amani endelevu na ulinzi na usalama katika maeneo yanayozunguka migodi ya Acacia yaliondaliwa na Shirika lisilo la Kiserikali la Search For Common Ground La Mjini Kahama.
Katika mafunzo hayo yaliojumuisha yaliojumuisha viongozi mbalimbali kutoka katika kata zilizo jirani na Migodi ya Dhahabu ya Bulyanhulu pamoja na Buzwagi yallikuwa na lengo la kuelimisha viongozi hao juu ya Sera ya ardhi ili kutokuleta mifarakano na wawekezaji.
Alisema kuwa migogoro mbalimbali inayotokea imekuwa ikisababishwa na kutoshirikishwa kwa Wananchi katika kutatua matatizo mbalimbali yanayohusika na ardhi hali ambayo inasababisha mifakano baina ya Mwekezaji na mmiliki wa ardhi wakati malipo ya fidia
Alisema
kuwa kwa sasa Wananchi lazima watambue Sheria na kanuni mbalimbali zinazohusu
masuala ya ardhi hali ambayo kwa kutumia viongozi hao walipata mafunzo wataweza
kuifikisha katika jamii husika kwa kutumia vikao mbalimbali au mikutano ya hadhara.
Aidha
alisema kuwa ushirikiano katika kutatua migogoro ya ardhi ni suala la msingi na
kuiongeza kuwa kufanya hivyo migogoro inaweza kutatuliwa huko huko katika eneo
husika kabla ya kufikishwa Mahakama za
ngazi ya juu.
Kwa
upande wake Meneja wa Shirika la Search for Common Ground Lazaro Mapimo alisema
kuwa Shirika lake linafanya kazi katika
nchi 34 Duniani na kuongeza kuwa katika ya Tanzania shirika hilo linafanya kazi
Wilayani Katika Mioigodi ya Acacia Bulyanhulu pamoja na Buzwagi, Mkoani Mara katikam Mgodi wa Norh Mara pamoja na
Visiwani Zanzibar.
Alisema
kuwa kwa muda wa miaka mitano tangu shirika hilo lianze kufanya kazi hapa
nchini limeweza kutoa mafunzo mbalimbali ya juu ya ujirani Mwema baina ya
Wananchi wanazunguka Migodi na tayari mafanikio yamekwishaanza kuonekana katika
maeneo mbalimbali kwani Wananchi
wameanza kujua stahiki zao.