Wednesday, June 17, 2015

JK AWAONGOZA MAELFU KUMZIKA MUFTI SIMBA

BOFYA HAPA CHINI KUONA MAAJABU YA LEO

Rais Jakaya Kikwete akiweka mchanga katika kaburi la Mufti Simba katika makaburi ya Nguzo nane mjini Shinyanga 
 RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete,amewaongoza maelfu ya waumini wa Dini ya kiislamu na watu wengine wenye imani mbalimbali,kumzika Sheikh Mkuu wa
Tanzania,Mufti Alhaji Sheikh Shaaban bin Simba katika makaburi ya Nguzo nane mjini Shinyanga.
WAZIRI Mkuu Mstaafu wa Serikali ya Awamu ya tatu,Fedrick Sumaye
 Maziko hayo yalifanyika jana baada ya mshuko wa sala ya Alaasiri na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wa dini ya kiislamu,wakristo na viongozi wa serikali ambao walijitokeza kumzika Mufti Simba aliyefariki dunia juzi akipatiwa matibabu kutokana na kusumbuliwa sana na sukari,Shinikizo la Damu (BP)  pamoja na Figo.
WAZIRI Mkuu aliyejiuzuru katika Serikali ya Awamu ya Nne,Edward Lowassa.
 Mwili wa marehemu uliwasili mchana mjini Shinyanga ukitokea jijini Dar es salaam na kufikishwa nyumbani kwa marehemu katika mtaa wa Majengo kata ya Kambarage katika manispaa ya Shinyanga.
WAZIRI wa Mambo ya Nje wa Tanzania,Benard Membe.

Baadaye mwili ulipelekwa katika msikiti wa  Masjidu Thaqafal Abdallah Islamiya uliopo Majengo mjini Shinyanga kwa ajili ya sala ya alasiri kisha mwili huo kupelekwa katika makaburi ya Nguzo Nane kwa ajili ya Maziko.

Kadhi mkuu wa Tanzania Sheikh Yusuph Bin Abdalla Mnyasi akiweka mchanga kwenye kaburi.
Pia watia nia mbalimbali wa nafasi za Uwakilishi katika majimbo ya mkoa wa Shinyanga wakiongozwa na Watia nia wanne wa urais Lazaro Nyalandu,Fredrick Sumaye,Edward Lowassa na Bernard Membe pia wamelihudhuria maziko hayo.

KUONA VIDEO MPYA BOFYA HAPA CHINI