Friday, March 27, 2015

WALIOACHISHWA AJIRA KATIKA UMRI MDOGO WALALAMIKA

BOFYA HAPA CHINI KUONA MAAJABU YA LEO

WANACHUO Dastan Dickson aliyesimama na Benjamin Paul.
VIJANA walioachishwa ajira migodini kutokana kuwa na umri mdogo kisha kupelekwa chuoni kupata elimu ya ufundi mbalimbali,wamedai elimu ya nadharia wanayopatiwa inawachanganya
hivyo ni vyema wakapatiwa ya vitendo itakayokidhi malengo stahiki ya kupata ujuzi,utakaokuwa mkombozi wa maisha yao.
MKURUGENZI wa HUHESO Foundation,Juma Mwesigwa,kulia.
Wakiongea mbele ya Uongozi wa Shirika la The Foundation for Human Health Society HUHESO FOUNDATION,ambao wanatekeleza kwa kushirikiana na mashirika matatu,kuwaondoa watoto wanaotumikishwa kazi ngumu katika migodi midogomidogo iliyo wilayani Kahama,vijana hao walidai kukabiliwa na changamoto nyingi chuoni hapo.
MKUU wa Chuo cha Wananchi Malampaka,Sospeter Kugasa.
Vijana hao 180,walisema tangu wamefika chuo cha VETA, cha Wananchi Malampaka,wamekuwa wakipatiwa mafunzo ya darasani huku wengi wao wakiwa hawajui kusoma na kuandika kutokana na kutowahi kupelekwa shuleni,hivyo kuona wanapoteza muda wao iwapo hawatapatiwa mafunzo kwa vitendo.
WANACHUO wa Taaluma ya Ufundi gari.
“Inashangaza kozi tulizoahidiwa hazipo,na kibaya Zaidi kwa wanaochukua ufundi wa kutengeneza magari wanawekwa darasani,ama kuonyeshwa vipuri kupitia magari mabovu yasiyotengenezeka yaliyopo chuoni,hawapati ujuzi ama uzoefu wowote ni vyema wangetafutiwa gereji ili kupata ufundi kwa vitendo,hali ni hiyo hiyo kwa wanaochukua ufundi wa umeme wa majumbani na viwandani”Alisema Richard Alex.
WANACHUO katika kikao na Uongozi wa HUHESO Foundation.
Aidha kwa wanaochukua ufundi wa kushona nguo,walilalamika uchache wa vyerehani uliopo chuoni usiolingana na idadi ya wanafunzi,sambamba nakutumia muda mwingi kutumikishwa shughuli nyingine za kijamii chuoni hapo badala kupatiwa mafunzo ya ufundi huo.
MWANAHABARI mtoto Irene akiwa katika mahojiano na wanachuo.

MWANACHUO Levania Adraham akitoa dukuduku lake.
Vijana hao pia walilalamikia suala la kupata maji safi na salama ambalo limekuwa ni tatizo kubwa kwao kiasi cha  kuathiri afya zao.

 Mkurugenzi wa Huheso Foundation,Juma Mwesigwa,aliwaomba vijana hao kuwa wavumilivu na kuwa changamoto zinazowakabili watazishughulikia kwa ushirikiano wa mashirika mwenza,mfadhili wa mradi Terre des Hommes pamoja na uongozi wa Chuo hicho.
WANACHUO katika mahojiano na Wana Habari Watoto.
Mwesigwa alisema ni budi wazingatie nidhamu kwa kuwa ndio msingi wa maendeleo yao,kwa kutoipoteza fursa hiyo waliyoipata kwaajili ya ukombozi wa maisha yao,na kuzingatia kwa bidii kile wanachofundishwa katika fani wanazosoma.
WANACHUO katika Kikao.
Kwa upande wake Mkuu wa Chuo Cha Wananchi Malampaka,Sospeter Kugasa,alikiri vijana hao wengi kuwa hawajui kusoma na kuandika,lakini wamewafundisha na baadhi yao wameanza kupata uelewa huo ambao ni msingi mkuu katika maisha.
MWANAHABARI mtoto Irene katika mahojiano.
Kugasa alisema pia walipata changamoto kubwa ya kuwaweka sawa kisaikolojia kwa vijana hao ambao walikuwa tayari walikuwa wameishazoea kupata pesa,huku wakifika chuoni na hofu kwa kudhani maisha ya shule ni ya kupewa adhabu,na kuwatoa hofu vijana hao kuwa watapatiwa mafunzo yanayostahiki.
MWALIMU Dotto Felician,akifundisha kwa vitendo namna ya kuchomelea vyuma.










KUONA VIDEO MPYA BOFYA HAPA CHINI