Friday, January 23, 2015

HALMASHAURI KAHAMA YAFUNGA KANISA KWA KUKOSA VYOO.

BOFYA HAPA CHINI KUONA MAAJABU YA LEO

MCHUNGAJI msaidizi Moses Daud aliyechuchumaa akijenga ukuta wa choo.
KANISA la Healing &Refugees Tanzania Church “HRTC” lililo Kata ya Nyihogo Mjini Kahama wilaya ya  Kahama mkoani Shinyanga limelifungwa na Halmasahuri ya mji wa Kahama baada
ya kubainika halina vyoo vya kujisaidia waumini wake.

Kwa mujibu wa barua iliyoandikwa na Kaimu Mkuu wa Idara wa Usafi na Mazingira katika Halmashauri hiyo ya Mji wa Kahama,Johannes Mwebesa,ilionesha Kanisa hilo alilifunga Desemba 29 mwaka jana,ingawa kufungwa rasmi lilifungwa na Polisi Januari 8,mwaka huu.
WAKISHIRIKI kujenga choo

Katika barua hiyo iliyosainiwa na Mwebesa na nakala kupelekwa kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Mji wa Kahama,ilieleza kulifunga  Kanisa hilo baada ya kubaini kufanya ibada zake bila kuwa na vyoo ambapo ni kinyume na sheria ya mazingira isiyoruhusu kukusanya watu bila kuwa na sehemu ya kujisaidia.

Hata hivyo uamuzi huo umepingwa na Wachungaji wa kanisa hilo;Moses Daud na Joshua Machibya ambao walidai uamuzi huo haujawatendea haki kutokana na nguvu kubwa iliyotumika kufunga Kanisa hilo kwa kutumia Polisi.
MCHUNGAJI Mkuu wa Kanisa la HRTC;Joshua Machibya akibeba tofari.

Mchungaji Msaidizi wa kansa hilo, Daud,alisema yeye na waumini wake walishangazwa na kitendo cha Halmashauri hiyo,kuwavamia na kufunga kanisa lao bila maelekezo yoyote ya ujenzi stahili wa vyoo.
Alidai wanavyofahamu  walipaswa kukaguliwa kisha kupewa maelekezo sambamba na muda wa ujenzi wa vyoo,hasa kwakuwa tayari waumini walikuwa na choo kingine cha muda walichokuwa wakitumia wakati taratibu za ujenzi zikiendelea, lakini walichofanya ni kufunga kanisa.
MCHUNGAJI Mkuu;Joshua Machibya kulia akimkabidhi tofari Mchungaji Msaidizi;Moses Daud,ili kuendelea na ujenzi.

Alisema pamoja na kufika ofisini kwao kwa ajili ya kuomba muda hawakusikilizwa na badala yake Januari 8,mwaka huu walifikiwa na Polisi kwa vitisho mbalimbali kama wao kazi wanayo ifanya kwa maslahi yao ambapo ni kwa maslahi ya kiroho.
WAKIENDELEA na Ujenzi wa Choo cha Wanawake.

Naye Mchungaji Machibya ambaye ndio Mchungaji Mkuu wa Kanisa hilo alisema kilichomshangaza yeye watumishi wa Idar ya Mazingira kuja na Polisi kuwakamata wakidai wamekaidi amri ya kulifunga Kanisa hilo,hali ambayo ilikuwa na vitisho vikubwa kinyume na taratibu za kibinadamu.
Naye Mwebesa Kaimu Idara ya Usafi na Mazingira katika Halmashauri hiyo,jana alipotakiwa kuzungumzia hali hiyo alikiri kulifunga kanisa hilo kwa madai yupo kisheria kutokana na Kanisa hilo kufanya shughuli zake bila kuwa na huduma ya vyoo kwa waumini wake.










KUONA VIDEO MPYA BOFYA HAPA CHINI