Sunday, December 21, 2014

ZIWA VICTORIA HATARINI KUTOWEKA

BOFYA HAPA CHINI KUONA MAAJABU YA LEO



IMEELEZWA kuwa ziwa Victoria liko katika hatari ya kutoweka katika ramani ya dunia kutokana na shughuli
mbalimbalii za binadamu zinazofanywa kando ya ziwa hilo.

Mtaalamu wa mazingira idara ya maji katika bonde la Ziwa Victoria, Wangasa Ogoma,alibainisha hali hiyo  hivi karibuni na kwamba maji yamekuwa yakishuka kina chake kila mwaka hali inayotishia usalama wa ziwa hilo.
 



Ogoma alisema shughuli hizo ni pamoja na kilimo na ujenzi unaofanywa ndani ya mita 60 kutoka katika ziwa hilo.

Nae mkurugenzi wa mazingira katika Ofisi ya Makamu wa  Rais Jijini Dar es salaam,Dk Julius Ningu,alisema kuna haja kwa kila mwananchi kuchukua hatua ya kupinga shughuli hizo kwa kushirikiana na serikali.

Aliongeza kuwa ziwa victoria  ni rasilimali muhumu kwa baadhi ya nchi zinazozungukwa na ziwa hilo hivyo linapaswa kulindwa kwa umakini zaidi.

KUONA VIDEO MPYA BOFYA HAPA CHINI