IMEELEZWA
kuwa uhaba wa upatikanaji bidhaa za biashara kutoka ndani ya wilaya Kahama
mkoani Shinyanga umechangia kwa kasi suala la mfumuko wa bei ya
bidhaa wilayani
humo.
Hayo yalisemwa na Katibu wa soko kuu mjini Kahama
Waziri Nyalubanda katika mahojiano na gazeti hili tando yaliyofanyika ofisini kwake,ambapo
alibainisha kuwa bidhaa nyingi kutoka nje ya wilaya zinasababisha kuwepo kwa mfumuko
wa bei.
Nyalubanda aliongeza kuwa bidhaa nyingi za kibiashara
hususani vyakula vimekuwa vikitoka nje ya wilaya na hata mkoa kwa ujumla jambo
linalopelekea bei kupanda kutokana na gharama za usafirishaji kwa
wafanyabiashara.
Kwa takwimu fupi ya bei ya mchele kwa kilo ni kati ya
shilingi1800 mpaka 2000 kilo ya maharage ni shilingi 2000 Dengu ni shilingi
1800,na bidhaa zinginezo jambo ambalo kwa wenye kipato cha chini inakuwa ni
vigumu kupata huduma.
Hata hivyo alisema taratibu za uongozi wa soko na
serikali wakishirikiana na wafanyabiashara ni kuboresha mzunguko wa bidhaa
sokoni hapo jambo ambalo litatoa unafuu wa gharama kwa wafanyabiashara na
wanunuzi wa bidhaa.
KUONA VIDEO MPYA BOFYA HAPA CHINI