Friday, December 26, 2014

WATOTO 18 WAZALIWA MKESHA WA KRISMASI KAHAMA

BOFYA HAPA CHINI KUONA MAAJABU YA LEO

JUMLA ya watoto kumi na nane wamezaliwa usiku wa mkesha wa sikuku ya Christmas katika hospitali ya wilaya ya Kahama mkoani shinyanga ambapo kati ya hao 10 ni wa kiume na wa kike 8

.


  Akizungumza
leo,Mganga Mfawidhi hospital ya wilaya ya Kahama Dkr,Charles Rwaikeza,alisema kuwa

jumla ya watoto kumi na nane wamezaliwa usiku wa mkesha wa sikuku ya Christmas wote wakiwa wamezaliwa salaama bila matatizo yoyote.
Dr.Rwaikeza alisema kuwa alipokea takwimu za watoto waliozaliwa kutoka kwa wakunga waliokuwa zamu ambapo ilikuwa jumla ya watoto kumi nane wamezaliwa wakiwa na afya njema sambamba na wazazi waliojifungua watoto hao wakiwa na siha njema.

Hata hivyo Rwaikeza aliwataka wakina mama waepuke kujifungulia nyumbani badala yake pindi wanapojihisi mabadiliko ya kimwili wakati wa ujauzito wawahi katika hospital ama zahati zilizo karibu nao ili kupata matibabu ikiwa ni njia mojawapo ya kujifungua salaama.


Aliongeza kuwa pindi wakina mama wajawazito wanapokuwa hospitalini wakisubiri wakati wa kujifungua na kupata usumbufu kutoka kwa wauguzi wasisite kufika katika ofsi ya mganga mfawidhi kwa lengo la kupatiwa ufumbuzi wa matatizo yanayokuwa yamejitokeza kwa wauguzi wa zamu.

KUONA VIDEO MPYA BOFYA HAPA CHINI