WANANCHI wa
mtaa wa Igalilimi Kata ya Kahama mjini wilayani Kahama
mkoani Shinyanga wametakiwa kuondoa makundi yaliyokuwepo wakati wa uchaguzi wa serikali za mitaa na badala yake waoneshe ushirikiano na viongozi waliochaguliwa ili kufikia maendeleo waliotarajia kwa wakati.
mkoani Shinyanga wametakiwa kuondoa makundi yaliyokuwepo wakati wa uchaguzi wa serikali za mitaa na badala yake waoneshe ushirikiano na viongozi waliochaguliwa ili kufikia maendeleo waliotarajia kwa wakati.
Mwenyekiti wa Mtaa huo Ibrahim Khan alisema hayo na kuomba juhudi
zilizooneshwa kwa umoja baina ya wananchi na viongozi wa vyama wakati wa kampeni za uchaguzi
zitakakiwa
kuhamishiwa katika kupigania maendeleo kwa kuwaunga mkono viongozi waliochaguliwa bila kujali itikadi ya vyama vyao.
kuhamishiwa katika kupigania maendeleo kwa kuwaunga mkono viongozi waliochaguliwa bila kujali itikadi ya vyama vyao.
Alisema kama
wananchi wataunganisha nguvu kwa kuonesha ushirikiano itasaidia mtaa huo kusonga
mbele kwa haraka kimaendeleo katika maeneo yote.
Katika hatua
nyingine Khan aliwashukuru wananchi wa mtaa huo kwa kumchagua kuwa mwenyekiti
ambapo ameahidi kuwa kwa kushirikiana na wajumbe wake watahakikisha wanafanya
kazi bila ya kuwepo kwa upendeleo wowote.
Aidha alisema
atahakikisha wanaboresha miundombinu hususani maeneo korofi ambapo kwa
kushirikana na halmashauri ya Mji na serikali wilayani humo watahakikisha
wanafanikisha kuboresha maeneo hayo.
Uchaguzi wa
serikali za Mitaa hufanyika kila baada ya miaka mitano ambapo mwaka huu
imefanyika disemba 14 licha ya kuwepo kwa dosari kadhaa ambazo zilifanya baadhi
ya maeneo kusogeza mbele kwa uchaguzi huo.
KUONA VIDEO MPYA BOFYA HAPA CHINI