Friday, December 12, 2014

WATANZANIA ELFU 11 KUPIGA KURA SERIKALI ZA MITAA

BOFYA HAPA CHINI KUONA MAAJABU YA LEO



Zikiwa zimebaki siku chache kabla ya kufanyika kwa uchaguzi wa serikali za mitaa, ofisi ya waziri mkuu TAMISEMI imetangaza jumla ta watanzania   11,491,661 wamejiandikisha na wanatarajiwa  kupiga kura.
Idadi hiyo ambayo ni
sawa na asilimia 62 ya matarajio ya watu 18,587,742 ambao walitarajiwa kuandikishwa kama asilimia 42 ya watanzania wote kwa mujibu wa sensa ya watu na makazi ya mwaka 2012.
Takwimu hizo zimetolewa na mkurugenzi wa uchaguzi wa serikali za mitaa Khalist Luanda wakati akizungumzia hali ya uchaguzi huo na maandalizi yake kwa ujumla hapa nchini.
Luanda amesema hadi leo maandalizi ya uchaguzi huo yalikuwa yakiendelea na kulikuwa na hali nzuri kwa maeneo yote nchini.
Mkurugenzi huyo amesema tayari halmashauri zote zimeshachapisha majina ya wagombea pamoja na nembo za halmashauri zao ambazo ndizo zitakazotumika kwa maeneo yote.
Kwa upande mwingine ameutangaza mkoa wa Katavi kuwa umeibuka kinara kwa kuandikisha wapiga kura kwa asilmia 79 ukifuatiwa na Kagera ambao uliandikisha kwa asilimia 78, wakati wilaya za Mpanda na Babati zikifanya vizuri kwa kati ya asilimia 107 (mpanda) na 101 kwa babati.
Mikoa iliyofanya vibaya ni Dar es salaam ambao uliandikisha kwa asilimia 43 na Kilimanjaro kwa asilimia 50 wakati wilaya zilizofanya vibaya ni Kilindi mkoani Tanga (21%) na wilaya ya  Same-Kilimanjaro iliandikisha kwa 22%.
Amesema kuwa TAMISEMI haijawa na takwimu sahihi za wagombea waliokuwa wameshindwa kuendelea na uchaguzi baada ya kuwekewa mapingamizi na kwamba bado wanafuatilia ili kujua wangapi wamewekewa mapingamizi hayo.

KUONA VIDEO MPYA BOFYA HAPA CHINI