Friday, December 12, 2014

WANA CCM GEITA WANUSURUKA KIFO

BOFYA HAPA CHINI KUONA MAAJABU YA LEO


WATU kumi ambao ni wafuasi wa chama cha mapinduzi, katika kata ya kalangalala Wilayani Geita,wamenusurika kuchomwa moto na wananchi wakati wakigawa chumvi ili kuwashawishi wananchi kuchagua viongozi wa chama hicho katika uchaguzi ujao wa serikali za mitaa.


Katika tukio hilo,vigogo wa CCM mkoa akiwemo mbunge wa viti maalumu Vicky Kamata, walifika eneo la tukio kwa lengo la kuwakingia kifua watuhumiwa hali iliyopelekea polisi kutishia kuondoka eneo hilo ili wananchi wajitawale.

Tukio hilo limetokea usiku wa kuamkia desemba 10,2014 saa 3.30 usiku na kulilazimu jeshi la polisi kutumia nguvu ya ziada kuwashawishi wananchi kutojichukulia sheria mkononi kwa kuwapiga na kuwachoma watu hao mbele ya vyombo vya dola.



Kufuatia zoezi hilo la ugawaji wa chumvi baadhi ya wananchi waliwapigia simu wanahabari ili kushuhudia tukio hilo na kwamba watuhumiwa hao walikuwa ndani ya nyumba ya balozi wa chama hicho wakati wa ugawaji huo.

 Kufuatia ghasia hizo polisi waliwataka vigogo hao wa CCM kuwa wapole huku wakitishia kuondoka eneo hilo ili wananchi wafanye watakavyo kutokana na vigogo hao kutaka kutumia vyeo vyao kuwafundisha kazi askari polisi.

 Aidha wanachama hao walifikishwa kituo cha polisi Wilaya ya Geita wakiwa na pakiti zao za chumvi ambazo walikuwa wakizigawa kwa wananchi.

Kwa mujibu wa mkuu wa upelelezi wa makosa ya jinai wilaya ya Geita John Maro, watuhumiwa hao wanashikiliwa na jeshi hilo kwa mahojiano zaidi na upelelezi ukikamilika watafikishwa mahakamani.

KUONA VIDEO MPYA BOFYA HAPA CHINI