Sunday, December 21, 2014

CHADEMA YAILETEA MTIKISIKO CCM MSALALA.

BOFYA HAPA CHINI KUONA MAAJABU YA LEO



HATIMAYE Halmashauri ya Msalala wilayani Kahama imekamilisha uchaguzi wake uliokuwa umekwama huku Chama cha Demokrasia na Maendeleo “CHADEMA” kikiuletea mtikisiko mkubwa Chama Cha Mapinduzi “CCM”kwa kutetea viti vyake na kupata vingine vilivyokuwa
katika himaya ya CCM.  

Kwa mujibu wa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo,Patrick Karangwa,alisema Uchaguzi huo umemalizika kwa  amani na utulivu ingawa kuna vitongoji vitatu mshindi ameshindwa kupatikana baada ya kura kulingana

Karangwa alisema CCM imeshinda kwa kupata nafasi 73 za vijiji kati ya 92 vilivyopo katika Halmashauri hiyo ya Msalala huku chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA kikipata nafasi 19 za vijiji. 

Aidha Karangwa alisema katika Halmashauri yake kuna Jumla ya vitongoji 390 ambapo CCM kimepata nafasi 299 huku CHADEMA wakipata 84 na UDP viwili pamoja na Chama Cha wananchi CUF kikipata kiti kimoja

Uchaguzi huo wa viongozi wa serikali za mitaa Jumapili iliyopita ulishindwa kufanyika ambapo mkurugenzi huyo alisema ni kutokana na sababu zilizokuwa nje ya uwezo wa  kiutendaji

Sababu zingine zilizoelezwa na Karangwa kukwamisha uchaguzi huo ni pamoja na umbali wa eneo la kiutawala na makao makuu ya Halmashauri hiyo ambapo siku hiyo magari ya kusambaza vifaa yalishindwa kufika kwa wakati kwenye vituo kutokana na mvua kubwa iliyonyesha na kuharibu barabara.

Hata hivyo Mwenyekiti wa CHADEMA wilaya ya Msalala,Emmanuel Bombeda alisema chama chake na washirika wake wa vyama vya UDP na CUF,wamekiletea mtikisiko mkubwa chama tawala kutokana na idadi ya viti walivyotwaa ambavyo ni mataji mkubwa kwa uchaguzi mkuu ujao.

“Hadi tunaenda kwenye uchaguzi wa Serikali za mitaa,tulikuwa na viti viwili tu ambavyo ni kuwa na Serikali ya Kijiji cha Kakola na Ilogi ambavyo tumevitetea na kuongeza vijiji vingine 17 vilivyokuwa chini ya CCM,na kwa upande wa vitongoji hatukuwanacho hata kimoja leo kwa ujumla wetu tunavyo 87,kwetu ni ushindi mkubwa,”alisema Bombeda.

Msalala ni moja ya Halmashauri tatu zinazounda wilaya ya Kahama ambazo mbali na hiyo pia zipo zingine mbili za Ushetu na mji wa Kahama ambazo Jumapili iliyopita zilifanya uchaguzi wake wa viongozi wa serikali za mitaa

KUONA VIDEO MPYA BOFYA HAPA CHINI