Sunday, December 21, 2014

MADIWANI CHATO WATAKA TAMISEMI ICHUNGUZE KIINI CHA KUHARIBIKA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA

BOFYA HAPA CHINI KUONA MAAJABU YA LEO



BAADHI  ya madiwani katika Halmashauri ya wilaya ya Chato,mkoani Geita wameiomba serikali kufanya
uchunguzi katika Halmashauri hiyo ili kufahamu kiini cha kuharibika kwa uchaguzi wa serikali za mitaa uliopita nchini.

Kauli hiyo ilitolewa  kwa nyakati tofauti na madiwani hao,huku wengi wao wakitaka waziri ofisi ya waziri mkuu serikali za mitaa na  tawala za mikoa TAMISEMI,Hawa Ghasia kumchukulia hatua haraka mkurugenzi wao Clement Belege

Kwa upande wake  Diwani wa kata ya Ilemela Ismail Luge alisema Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo ameharibu uchaguzi kwa kushindwa kuchapisha karatasi za kupigia kura wajumbe na badala yake wananchi walipiga kwa kuandika majina kinyume na taratibu

Luge alisema hali hiyo imefanya zoezi kuwa gumu  kwa wananchi ambao hawajui kuandika hali ambayo kwa kawaida majina huchapwa kwenye karatasi hiyo ambayo wananchi huweka vema kwa mtu wanayemtaka hali ambayo mkurugenzi huyo hakufanya hivyo

Kwa upande wake Belege alipotakiwa kuzungumzia hali hiyo alisema swala hilo haliwezi kuzungumzwa kwa ufupi bali linahitaji Maelezo marefu juu ya taratibu zilizotumika kuchapisha karatasi hizo

Madiwani wengine wanaotaka Ghasia amchukulie hatua mkurugenzi huyo ni  Eramu Lubagola wa kata ya Bwela Stela Kiwanuko wa kata ya Kachwamba Abel Chamwanda wa kata ya Makurugusi pamoja na Marco Maduka wa kata ya Mganza wanaodai kwa pamoja mkurugenzi huyo amevuruga uchaguzi huo.

Chanzo cha habari ni Shija Felician,Chato.

KUONA VIDEO MPYA BOFYA HAPA CHINI