![]() |
WAZIRI wa Maji na Umwagiliaji,Profesa Jumanne Maghembe |
WAKATI Mzimu wa Akaunti ya Tegeta Escrow ungali
ukiitesa Serikali,Wajumbe wa Bodi ya Mamlaka ya Maji safi na Usafi wa Mazingira
katika mji wa Kahama mkoani Shinyanga “KUWASA”wanachunguzwa na TAKUKURU wilayani
Kahama,kwa ubadhirifu wa Shilingi Milioni 3.6.
Maamuzi hayo ya bodi ya KUWASA yamewaingiza
matatani wajumbe wake baada ya Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Tanzania wilayani
Kahama,kuanza kuwahoji juu ya uamuzi huo sambamba na matumizi mabovu ya
Madaraka waliyokasimishwa.
Hali hiyo ilibainishwa Desemba 24,mwaka huu
katika Ofisi za KUWASA,na Mwenyekiti wa bodi hiyo,Boniphance Lutege wakati
akiongea na waandishi wa habari muda mchache mara baada ya TAKUKURU,kuwahoji na kuchunguza tuhuma
zinazowakabili wajumbe hao pamoja na meneja wa mamlaka hiyo Joel Rugemalila.
Kabla ya hapo mkuu wa TAKUKURU wilaya ya Kahama
Enock Ngailo alisema Taasisi yake inawahoji wajumbe wanane wa mamlaka
hiyo kwa tuhuma za maamuzi ya ukiukaji wa sheria na Matumizi mabaya ya bodi
hiyo hali ambayo inaweza kuzaa tuhuma zingine wakati wa uchugunzi .
Ngailo alisema mamlaka hiyo inatuhumiwa
kufanya maamuzi bila kufuata kanuni na taaratibu za kisheria kifungu namba 30
cha makosa ya rushwa,ingawa alisema hivi sasa tasisi yake iko katika hatua ya
awali ya uchunguzi juu ya Wajumbe wa Bodi ya KUWASA.
Hata hivyo alidai katika uchunguzi kuna mambo
mengi yanayoweza kuibuka ikiwemo ubadhirifu wa mali ya umma na mengineyo ingawa
Taasisi yake katika hatua ya awali inachunguza tuhuma mbili za Matumizi ya maamuzi
ya mamlaka ya kujiongezea posho ya vikao kwa siku bila kufuata taratibu za
kisheria na utata wa ajira unao
husisha bodi hiyo.
Kufuatia hali hiyo Lutege alikiri bodi yake
kuchuguzwa na TAKUKURU huku akisema kinacholenga wajumbe wake moja kwa
moja ni maamuzi ya kupandisha posho ya vikao kutoka shilingi laki tatu
mpaka laki nne na nusu kwa siku huku tuhuma ya ajira akimtupia meneja wake Joel
Rugemalila.
Katika hilo Lutege alifafanua,wakati bodi hiyo
haijaundwa baada ya iliyokuwepo kumaliza muda wake Rugemalila kupitia uongozi
wake waliajiri watumishi wawili katika nafasi za Afisa mahusiano na afisa
utumishi bila kupitia bodi kinyume na kanuni na taratibu za kisheria za
ajira
Pamoja na hali hiyo Lutege alisema kwa kuwa
tayari swala hilo liko TAKUKURU hivyo ni wajibu wa taasisi hiyo kufanya kazi
yake ya uchunguzi na baada ya hapo tuhuma hizo zitabainishwa kisheria
Mamlaka hiyo imekuwa ikikumbwa na kashfa
mbalimbali za kiutawala ambapo Taasisi hiyo ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa mara
nyingi imekuwa ikiwahoji juu ya tuhuma hizo,lakini inaonyesha haijapa ufumbuzi
wa tuhuma za kiutawala za mamlaka hiyo.
KUONA VIDEO MPYA BOFYA HAPA CHINI