Sunday, December 28, 2014

KIKONGWE CHADAIWA KUDONDOKA NA UNGO KAHAMA

BOFYA HAPA CHINI KUONA MAAJABU YA LEO


WAKAZI wa Bukondamoyo katika Halmashauri ya mji wa Kahama mkoani Shinyanga wameingiwa na hofu baada ya bibi kizee  mmoja kudaiwa kudondoka kwenye ungo akidaiwa kutoka mkoani Tabora kusherekea sikukuu ya Chrismas
 
Kwa mujibu wa watu walioshuhudia tukio hilo lililokusanya umati mkubwa wa watu wamedai bibi kizee huyo alidondoka alfajiri huku akidai alikuwa na wenzie watano ambao walifanikiwa kutoroka kuelekea kijiji cha Ndugu kata ya Kinaga wilayani Kahama
 
Aidha bibi kizee huyo baada ya kuhojiwa na hili gazeti tando alisema anaitwa Chausiku huku akidai alikuwa akielekea katika kijiji hicho cha ndugu
 
Hata hivyo jeshi la polisi wilayani Kahama liliwahi kufika kwenye tukio na kumuokoa bibi kizee huyo ambaye alionekana kuvaa nguo zilizochakaa na makovu katika mkono wake wa kushoto ambapo imedaiwa alichubuka wakati akidondoka
 
Tukio hilo limehusishwa na imani za kishirikina kwa kuwa ungo ni kifaa kinachoaminiwa kutumika kwa nguvu ya giza kupaa angani kama usafiri unaotumiwa na wanga katika shughuli zao za nguvu ya giza  ikiwemo uchawi
 
Na Shija Felician - Kahama.

KUONA VIDEO MPYA BOFYA HAPA CHINI