Friday, November 14, 2014

WATU ELFU TANO WAFARIKI KWA EBOLA AFRIKA MAGHARIBI

BOFYA HAPA CHINI KUONA MAAJABU YA LEO

 SHIRIKA la Afya Duniani (WHO) limetangaza kuwa, idadi ya watu waliofariki duniani kutokana na mfumuko wa ugonjwa wa homa ya Ebola huko Magharibi mwa Afrika imeongezeka na kufikia 5,147 huku watu
wengine 14,068 wakiambukizwa ugonjwa huo.

 WHO imeongeza kuwa, vifo vingine 13 na watu 30 wameambukiwa katika nchi 5 za Nigeria, Senegal, Mali, Uhispania na Marekani.
 
Shirika hilo limeongeza kuwa, maambukizo ya ugomjwa huo yamepungua katika nchi za Guinea na Liberia lakini yameendelea kuongezeka huko Sierra Leone ambako kumeripotiwa kesi mpya 421 za maambukizi katika wiki moja hadi kufikia Novemba 9.

Wataalamu wa afya walisema, idadi ya kesi mpya ni muhimu sana kuliko wanaokufa kutoka na ugonjwa huo, kwani inaakisi jinsi virusi vya Ebola vinavyosambaa.  

Watu wasiopungua 75 waliwekwa katantini katika mji mkuu wa Mali, Bamako baada ya kufariki dunia muuguzi mmoja aliyekuwa na ugonjwa huo.



Wakati huo huo shirika la Madaktari wasio na mipaka, MSF limesema litafanya majaribio ya tiba mpya ya Ebola katika vituo vitatu Afrika Magharibi.
 
Wafanyakazi hao watatumia dawa aina mbili zilizoainishwa na Shirika la Afya duniani, WHO.

Sababu ya kufanyika kwa majaribio hayo ni kuwafanya Wagonjwa kuendelea kuwa hai wakati wa siku 14 za mwanzo tangu maambukizi ya ugonjwa huo.

CHANZO cha Habari ni Tehran swahili &BBC

KUONA VIDEO MPYA BOFYA HAPA CHINI