Friday, November 14, 2014

WANAO WAONGOZA WATALII WAFUNDWA

BOFYA HAPA CHINI KUONA MAAJABU YA LEO


WAONGOZA watalii nchini wametakiwa kuhakikisha kuwa wanasaini mikataba halali ya kazi na wamiliki wa makampuni wanayofanyia kazi ili kuepuka kunyonywa haki zao.




Rai hiyo ilitolewa na Naibu Waziri wa Maliasili na Utaliii, Mahmoud Mgimwa katika mkutano mkuu wa mwaka wa chama cha waongoza watalii mlima Kilimanjaro kilichofanyika mjini Moshi mkoani Kilimanjaro.




Alisema, hifadhi ya mlima Kilimanjaro ndiyo hifadhi inaingizia serikali mapato makubwa ikilinganishwa na hifadhi nyingine, hivyo kuwataka waongoza watalii kufanya kazi kwa umakini kwani kutofanya hivyo watalikosesha taifa mapato yatokanayo na utalii katika mlima huo.



Aliwaahidi waongoza watalii hao kuwa, atakutana na chama cha wamiliki wa makapuni ya utalii nchini pamoja na chama cha wamiliki wa makampuni ya utalii Kilimanjaro ili kuona namna ya kulinda maslahi ya waongoza watalii.



Kwa upande wake mkuu wa hifadhi ya KINAPA, Erasto Lufungulo, alisema waongoza watalii wamekuwa sehemu kubwa katika kuyatunza mazingira ya hifadhi ya mlima huo.

KUONA VIDEO MPYA BOFYA HAPA CHINI