Friday, November 14, 2014

WANANCHI WAPINGA KUMPISHA MWEKEZAJI

BOFYA HAPA CHINI KUONA MAAJABU YA LEO



WANANCHI wa Kijiji cha Kanegere kata ya Bukandwe Wilaya Mbogwe Mkoani Geita wameiomba Serikali kuingilia kati kupinga kitendo cha Mwekezaji kuwapatia wananchi  Notisi ya kuhama kijijini hapo ili kupisha shughuli za utafiti wa madini kijijin hapo.

Wakiongea na Wandishi wa Habari, Wananchi hao walisema kitendo kilichofanywa na mwekezaji huyo sio cha
kiungwana kwani kaya zilizopo Kijijini humo zipo kwa muda mrefu na kuwaondoa bila kufuata sheria ni kukiuka haki za kibinaadamu.

Walisema  Mtafiti huyo yupo tangu muda mrefu na haieleweki anatafiti nini na hata katika shughuli za kijamii amekuwa akikwepa kuchangia katika masuala mbalimbali ya kimaendeleo katika kijiji hicho zaidi ya kuwafukuza wachimbaji wadogo wanaochimba dhahabu.

Mmoja wa Wachimbaji hao Zacharia Maghembe alisema Mwekezaji huyo yupo katika eneo hilo kwa miaka 22 ambapo anachokifanya ni kubadilisha makumpuni ya utafiti na kuzuia shughuli za mendeleo  katika kijiji hicho akidai maeneo hayo ni yake.

Akijibu  tuhumza hizo Meneja utafiti wa Kampuni ya Mabangu Mining Limited William Harmsworth amekiri kwa kuwafukuza wachimbaji hao katika maeneo hayo ili kupisha ujenzi wa mgodi huo.

Harmsworth alisema Kampuni hiyo inawataka wananchi wote katika Kijiji hicho kuhama mapema iwezekanavyo kupisha ujenzi wa Mgodi unatarajiwa kuanza wakati wowote katika eneo hilo huku kukiwa hakuna ushahidi wa mwekezaji huyo kuwa na leseni ya uchimbaji.

Alisema Mabangu Mining Limited itafanya upembuzi yakinifu katika eneo hilo  ili kumlipa kila Mwananchi anayeishi katika Kijiji hicho kulingana na eneo lake na thamani ya nyumba anayoishi ili kupisha shughuli za uchimbaji kabla ya kuanza.

KUONA VIDEO MPYA BOFYA HAPA CHINI