Monday, November 10, 2014

SIMBA YAONDOA MZIMU WA SARE. OKWI AIVUA SIMBA KOTI LA SARE

BOFYA HAPA CHINI KUONA MAAJABU YA LEO


 EMMANUEL Okwi akongoza wenzake kushangilia bao.
GIZA lilotawaliwa na Mzimu wa sare katika Klabu ya Simba Sport Club huenda likawa limemalizika kutokana na matokeo iliyoyapata katika Mchezo wake wa Saba wa Michuano ya Ligi Kuu baada ya kuibanjua Ruvu Shooting bao 1 – 0.

Alikuwa ni Mshambuliaji wake
Raia wa Uganda Emmanuel Okwi ambaye alicheza mchezo wake wa nne ilhali akiwa mgonjwa ndio aliyeivua klabu yake koti lenye mzimu wa sare kwa kuipachikia bao mnamo dakika ya 79,kwenye uwanja wa Taifa Jijini Dar Es Salaam.
Okwi anaifungia Simba bao baada ya kuumiliki mpira mbele ya mabeki wa Ruvu Shooting na kutoa pasi kwa Maguri aliyepiga shuti kali, kipa Shooting Abdallah Rashid akatema na Okwi akamalizia wavuni.

Baada ya bao hilo Okwi alikimbilia kushangalia katika jukwaa la Yanga ambapo mashabiki wa watani hao muda wote wa mchezo walikuwa wakimzomea kwenda kuwaziba mdomo ambao nao walimrushia chupa za maji.

Ushindi huo wa kwanza katika Ligi kwa msimu huu pia na kwa uongozi wa Rais Aveva umeifanya timu hiyo kufikisha pointi Tisa baada ya kutoka suluhu mechi sita.

Katika pambano hilo lilionyesha dhahiri Simba kuibuka na ushindi kutokana na kucheza mchezo wenye malengo lakini kikwazo kilikuwa maafande hao ambao walionyesha umakini mkubwa katika kudhibiti mashambulizi ya Simba iliyopata kona Tisa huku Shooting ikiwa haijapata hata moja.



 MASHABIKI wa Simba wakishangilia ushindi wao wa kwanza.


 Baada ya Dakika 90 za mchezo kocha wa Simba Patrick Phiri akiwa mwenye furaha alidai ushindi huo unatokana na kikosi chake kuimarika sikua hadi siku,huku kocha wa maafande wa Ruvu Shooting, Tom Olaba akisema timu yake ilicheza vizuri isipokuwa haikutumia vyema nafasi ilizopata.

Nazo timu za Mtibwa Sugar na Kagera Sugar, zilihitimisha  kiporo chao cha pili kwa kutoka sare ya bao 1-1.

Ikumbukwe katika mchezo wa siku ya Jumamosi ambao ulivunjika wakati Mtibwa Sugar ikiongoza kwa bao 1-0 lililofungwa na Ame Ali.

Lakini mvua kubwa ikalazimu pambano liahirishwe na leo asubuhi kwenye uwanja wa Manungu, dakika 45 zilizobaki zikamaliziwa.

Kagera ikapata bao lake kusawazisha kupitia kwa Rashidi Mandawa katika dakika ya 57.

Sare hiyo ni ya tatu kwa Mtibwa Sugar ambayo imeshinda mara nne na kuendelea kubaki kileleni.

KUONA VIDEO MPYA BOFYA HAPA CHINI