Sunday, November 9, 2014

WAKULIMA WA PAMBA KAHAMA WAFUNDWA.

BOFYA HAPA CHINI KUONA MAAJABU YA LEO




WAKULIMA wa zao la pamba wilayani Kahama mkoani Shinyanga wametakiwa kufuata sheria kumi za uzalishaji wa zao hilo ili kupata pamba itakayokuwa na ubora zaidi.


 Meneja wa kampuni ya ununuzi na uchambuaji wa pamba (KCCL) Bahati Bayala alisema  wamekuwa wakikumbana na changamoto nyingi kutokana na wakulima kutokuwa na uelewa juu ya kilimo cha pamba hasa kutozingatia kanuni la zao hilo.

Alisema kuwa serikali inalo jukumu la kuwaelimisha wakulima wa zao hilo kupitia Mabwana Shamba ambao ndio walengwa watakaoweza kuwapatia elimu wakulima wa zao hilo juu ya uandaaji pamoja na uvunaji.

Kwa upande wake Meneja wa kampuni ya NIDA Gregory Kabuta alisema iwapo wakulima wa zao hilo watazingatia kanuni za kilimo bora za pamba ikiwa ni pamoja na kutumia mbolea za samadi kutasaidia kupata pamba yenye ubora zaidi.

Kabuta alisema suala la ugawaji wa mbegu wamezigawa katika maeneo mbalimbali huku wakiwahamasisha wakulima kujiaandaa na msimu wa mwaka 2014 na 2015.

Aliwataka wakulima kuzingatia utunzaji wa mashamba, na kuwakumbusha wakulima kutochanganya maji na  mchanga kwenye pamba kwa lengo la kuzidisha kilo hali ambayo inapunguza ubora wa zao la pamba.


KUONA VIDEO MPYA BOFYA HAPA CHINI