Tuesday, November 11, 2014

SERIKALI KUKOMESHA WIZI WA MAGARI BANDARINI.

BOFYA HAPA CHINI KUONA MAAJABU YA LEO


 
 NAIBU Waziri wa Uchukuzi Dkt.Charles John Tizeba akiongea.
SERIKALI imedhamiria kukomesha vitendo vya wizi wa vifaa mbalimbali vya magari bandarini kwa kuandaa mkakati maalumu utakaosaidia kutambua wahusika wafanyao vitendo hivyo vinavyolitia doa Taifa.


Hayo yalibainishwa na Naibu Waziri wa Uchukuzi Dkt.Charles John Tizeba ambapo alibainisha kuwa serikali imeweka dhamira ya dhati kutokomeza vitendo hivyo ambavyo kwa kipindi kirefu vimekuwa vikilalamikiwa na watu wanaoagiza na kusafirisha magari yao kwa njia ya maji.
 


Dkt.Tizeba alisema  imekuwa kawaida watu wengi kulalamikia vitendo vya wizi wa vifaa mbalimbali katika magari eneo la bandari ya Dar es Salaam, hatua ambayo imesababisha Serikali kutoa tamko rasmi juu ya mkakati unaoandaliwa ili kukomesha wizi huo.

Akizungumzia juu ya kukabiliana na vitendo vya wizi wa vifaa vya magari bandarini Naibu Waziri huyo alisema pamoja na kwamba jitihada zilizokwishafanyika zimepunguza uhalifu huo lakini lengo ni kuhakikisha vitendo hivyo vinatokomezwa kabisa.
 Dkt.Tizeba akisisitiza jambo kwa uongozi wa Wizara,Bandari na Mkurugenzi Mtendaji wa kitengo cha Kupakia na Kupakua Makontena TICTS;Neville Bisett.
Alifafanua katika mkakati ulioandaliwa ni kuwepo kwa mfumo unaoendana na teknolojia ya kisasa ambayo itakayohakikisha inatambua kasoro zilizo kwenye gari kabla halijatolewa katika meli.

Aidha alisema baada ya kufahamu kasoro hiyo,pia mfumo huo utaendelea kubaini mapungufu mengine baada ya gari hilo kushushwa toka katika meli na siku ya kuchukuliwa na mmiliki mwenyewe hivyo kama itaonekana na kasoro na kubainika tatizo hilo lilijitokeza kipindi gani na wapi.

 Alisema kupitia mkakati huo hakuna udanganyifu na uhalifu utakaofanyika pasipo wahusika kubainika hali ambayo itasaidia kukomesha matukio hayo ya wizi wa vipuri vya magari hasa kwakuwa wahalifu wake watapatikana na kuchukuliwa hatua kali za kisheria.

Kumekuwa na vitendo vya wizi unaosababisha upungufu wa vipuri vya magari yanayoagizwa kutoka ng’ambo jambo ambalo limekuwa likipigiwa kelele na wadau mbalimbali wanaoagiza magari ughaibuni.









KUONA VIDEO MPYA BOFYA HAPA CHINI