Friday, October 24, 2014

WANAFUNZI WAFANYA MITIHANI WAKIWA WAJAWAZITO

BOFYA HAPA CHINI KUONA MAAJABU YA LEO



IMEBAINIKA kuwa wanafunzi wa kike 53 nchini Kenya wanaofanya mitihani ya kumaliza Kidato cha nne ni wajawazito.

Kubainika huko kumekuja kutokana na taarifa iliyotolewa na Afisa Elimu katika Kaunti ya Bungoma Kenya,iliyotaja idadi
hiyo ya wanafunzi wanaofanya mitihani ya kuhitimu elimu ya sekondari iliyoanza siku ya Jumanne wiki hii ni Wajawazito.

Katika taarifa yake Mkurugenzi wa Elimu wa Kaunti hiyo;Charles Anyika iliyochapishwa na News 24 Kenya,imesema huenda idadi hiyo ikawa ni ndogo.

Taarifa hiyo ilibainisha kuwa uchunguzi uliofanyika katika eneo dogo umefaulu kutambua hali hiyo,ambapo inategemea kwa mazingira halisi na ukubwa wa eneo la nchi hiyo idadi ya wanafunzi wenye ujauzito inaweza kuwa kubwa zaidi.

Ufafanuzi ulieleza kuwa inategemea kuwa idadi ya idadi ya wanafunzi wenye ujauzito ikawa ni kubwa kuliko iliyopatikana kwa kuwa baadhi ya wakuu wa shule walitoa taarifa za uongo na pia baadhi ya familia wamekuwa ‘wakimalizana’ na watuhumiwa bila ya kutoa taarifa.

Anyika alisema awali kabla ya uchunguzi huo walitegemea idadi ya wanafunzi wenye mimba kufikia 100, wakati huo huo amewataka walimu wawaache wanafunzi hao wafanye mitihani yao kwa utulivu na kuwaagiza walimu kuandaa magari ambayo yatasaidia iwapo mwanafunzi yoyote atapata dharura.

Aidha aliwataja walimu, waendesha ‘bodaboda’, na wanaume waliooa ni wahusika wa mimba hizo na kuongeza kuwa umaskini ni chanzo kikubwa cha tatizo hilo, na kuwataka wazazi kuwalinda watoto wao na kuwapa elimu juu ya hatari ya mimba za utotoni pamoja na ngono zembe.

KUONA VIDEO MPYA BOFYA HAPA CHINI