Friday, October 24, 2014

BOKO HARAM YAFANYA UTEKAJI TENA NIGERIA

BOFYA HAPA CHINI KUONA MAAJABU YA LEO



WAKATI Serikali ya Nigeria ikihaha kuwapata na kuwarejesha kwa wazazi na walezi wao wasichana waliotekwa
na Wapiganaji wa Boko Haram,kikundi hicho cha wapiganaji kimefanya mashambulizi na kufanikiwa kufanya utekaji mwingine mkubwa wa binadamu.




Kwa mujibu wa taarifa iliyoripotiwa na Shirika la la Utangazaji Uingereza “BBC” imeeleza kwamba kikundi cha wapiganaji cha Boko Haram kimefanya mashambulizi katika kijiji cha Adamawa kilichopo Kaskazini Magharibi ya Nigeria na kuteka wanawake na wasichana katika kijiji hicho.
 



Boko Haram waliahidi kuwaachilia huru zaidi ya wasichana 200 wanaoshikiliwa na kikundi hicho,lakini badala ya kutekeleza ahadi hiyo,wamefanya utekaji wa wasichana na wanawake hao ikiwa ni siku sita tangu serikali ya Nigeria na kikundi hicho walipofanya makubaliano hayo.





Hata hivyo japo Boko Haram wamekiuka makubaliano waliyoafikiana Ijumaa iliyopita, bado serikali ya Nigeria ina matumaini ya kuachiliwa huru kwa wasichana hao baada ya kikao kinachotarajiwa kufanyika muda wowote kuanzia sasa huko Chad.

KUONA VIDEO MPYA BOFYA HAPA CHINI