Tuesday, October 7, 2014

SEKONDARI YA ANDERLEK RIDGES YATUMIA SHILINGI MILIONI 83 KUHIFADHI MAZINGIRA

BOFYA HAPA CHINI KUONA MAAJABU YA LEO

MKURUGENZI wa Taasisi ya Rocken Hill Academy inayomiliki Shule ya Sekondari ya Anderlek Ridges,Mr. Alexander Kazmil kwa bashasha akinyanyua kombe la ushindi wa Uhifadhi Mazingira kwa Shule za Sekondari Nchini alilokabidhiwa kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano Tanzania na Kiongozi wa Mbio za Mwenge Kitaifa 2014,Rachel Stephen Kassanda




SHULE ya Sekondari ya Anderlek Ridges iliyo katika Halmashauri ya Mji wa Kahama imetumia kiasi cha Shilingi Milioni 83,500,000/= kupanda jumla ya miti 9356 katika eneo la Shule ili
kuhakikisha inatunza vyema mazingira ya shule na kufanikisha kutoa na kupata elimu bora kwa vijana watakaobahatika kusoma shuleni hapo.

 KIONGOZI wa mbio za Mwenge Kitaifa 2014,Rachel Stephen Kassandaakizindua Klabu ya Malihai inayojihusisha na utunzaji mazingira katika Shule ya Sekondari ya Anderlek Ridges.

 KIONGOZI wa mbio za Mwenge Kitaifa 2014,Rachel Stephen Kassandaakipanda Mti shule ya Sekondari Anderlek Ridges.



Kwa mujibu wa Taarifa iliyosomwa mbele ya kiongozi wa Mbio za Mwenge Kitaifa kwa mwaka 2014,Rachel Stephen Kassanda na katibu wa Klabu ya Mazingira shuleni hapo Onesmo Nicholus,alisema katika idadi ya miti hiyo,miti 3400 waliipanda baina ya mwaka 2012 hadi 2014.

 KATIBU wa Kalabu ya Mazingira katika Shule ya Sekondari ya Anderlek,Onesmo Nicholaus,akimkabidhi Kiongozi wa Mbio za Mwenge Kitaifa 2014,Rachel Stephen Kassanda ,Taarifa aliyosoma ya Klabu ya Mazingira Shuleni hapo.Kushoto kwa Kiongozi wa Mbio za Mwenge ni Mkuu wa wilaya ya Kahama na kulia kwa Kiongozi wa Mbio za Mwenge ni Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Mji wa Kahama.



Nicholaus alisema Klabu ya Mazingira Shuleni hapo ilianzishwa mwaka 2010 ikiwa na wanachama 30 wakiwa ni wanafunzi wa kidato cha kwanza hadi cha nne na kwa sasa ina wanachama 54 wakiwa katika uwiano sawa baina ya wavulana na wasichana,ambapo amajukumu yao makubwa mbali na masomo ni kuratibu na kusimamia utunzaji wa mazingira ya shule ili kuwa bora kwa kutoa na kupata elimu.

  MKURUGENZI wa Shule ya Sekondari ya Anderlek,Mr.Alexander Kazmil kwa bashasha akilinyanyua juu Kombe la Tuzo ya Rais Mazingira baada ya Shule yake kushika nafasi ya kwanza katika shindano lililoshirikisha Shule za sekondari Nchini.


Alisema Klabu hiyo pia inajihusisha na kuelimisha jamii kuhusu athari za moto na namna ya kukabiliana nazo,kutoa elimu ya mabadiriko ya tabia nchi,elimu ambayo wanaipata hapo shuleni na kuahidi kuiendeleza hata mara baada ya kuondoka katika familia ya shule hiyo.

 MKURUGENZI wa Shule ya Sekondari ya Anderlek,Mr.Alexander Kazmil akipokea kikombe cha Tuzo ya Rais Mazingira,kutoka kwa Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa kwa mwaka 2014,Rachel Kassanda.



“Tunafurahi kupata bahati ya kujifunza kwa vitendo na kushiriki katika shughuli za utunzaji wa mazingira na upandaji miti,tunaahidi kuendeleza jitihada hizi za utunzaji mazingira na upandaji miti popote pale duniani mara baada ya masomo yetu”,alise Nicholaus.

 VIJANA wa Shule ya Sekondari ya Anderlek Ridges wakiwa katika mstari huku wakiimba kwa furaha wakati wa mapokezi ya Mwenge.


Aidha kwa upande wake Kiongozi wa Mbio zza Mwenge Kitaifa kwa mwaka 2014,Rachel Stephen Kassanda aliupongeza uongozi wa shule hiyo kuonyesha unafundisha kwa vitendo mambo muhimu yenye ustawi kwa Taifa kama utunzaji wa mazingira na upandaji miti.

 KIONGOZI wa mbio za Mwenge Kitaifa 2014,Rachel Stephen Kassanda akikagua vifaa vya kuhifadhia taka.


Kassanda alisema elimu wanayopata na kushiriki kwa vitendo kwa wanafunzi katika utunzaji wa mazingira itakuwa msaada mkubwa kuondokana na uharibifu wa mazingira katika jamii ya Watanzania hivyo kutoa wito kwa shule zote nchini kuhakikisha zinaanzisha klabu za mazingira hatua itakayosaidia kulirejesha taifa katika uoto wa kijani.

KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa 2014,Rachel Stephen Kassanda akiwa amekamatia Mwenge katika picha ya pamoja na uongozi wa Shule ya Sekondari ya Anderlek,sambamba na viongozi wa Klabu ya Mazingira ya Shuleni hapo.


Shule ya Sekondari ya Anderlek Ridges imefanikiwa kutwaa Tuzo ya Rais ya Usafi na Utunzaji Mazingira kwa mwaka 2013/2014 kwa shule za sekondari nchini baada ya kushika nafasi ya kwanza Tanzania bara na kupatiwa Cheti na hundi ya ShilingiMilioni Tatu.  

KUONA VIDEO MPYA BOFYA HAPA CHINI