Saturday, September 27, 2014

WATENDAJI KATA WAAGIZWA KUSIMAMIA KESI ZA MIMBA ZA UTOTONI

BOFYA HAPA CHINI KUONA MAAJABU YA LEO



KATIKA kutokomeza ubakaji na mimba za utotoni kwa wanafunzi sambamba na  kupata matokeo mazuri ya mwenendo wa kesi wa
vitendo hivyo,Maafisa Watendaji wa kata Wilayani Kahama wametakiwa kuwa mstari wa mbele  kusimamia kesi hizo badala ya kuwaachia wazazi jukumu hilo.



Agizo hilo lilitolewa na Mkuu wa Wilaya ya Kahama Benson Mpesya  wakati akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake kuhusu kesi ya mimba inayomkabili Masanja Julius {35} anayetuhumiwa kumpa ujauzito mwaka 2013 msichana mmoja aliyekuwa mwanafunzi wa darasa la saba  katika shule ya msingi Igwamanoni B kata ya Bugarama huku kesi hiyo ikionyesha kuwa na mwenendo usioridhisha toka ifunguliwe.



Mpesya alisema kuwa Maafisa Watendaji wa kata wamekuwa hawawajibiki vizuri ili kuhakikisha yanapatikana matokeo mazuri ya mwenendo wa kesi hizo kwa kuwaachia wazazi jukumu la kufuatilia kesi za Wanafunzi hao zinapotokea huku wakijua kuwa wao ndio wahusika wakuu wa kusimamia kesi hizo.



Alifafanua  kuwa kwa mujibu wa  sheria namba 19 ya ubakaji pamoja na ile namba 29 ya Elimu zote zinapinga mimba kwa wanafunzi hivyo kuwaagiza maafisa Watendaji wa kata kuzitekeleza vyema sheria hizo kwa kuwa wasimamizi waadirifu  katika kesi hizo zinawakabili wanafunzi wanapopewa mimba wakiwa bado shuleni kwa kuzisimamia hadi kuhakikisha zinamalizika kwa kuleta matokeo mazuri.



Mkuu huyo wa Wilaya aliwataka Watendaji hao kuongeza hali ya kuthamni Elimu na kuongeza kuwa kwa kufanya hivyo wanaweza kuisaidia Serikali katika kutimiza malengo yake na kuwataka kujua suala la kukataa ukweli mahakamani na kupoteza ushahidi vinaonyesha mianya ya Rushwa kwao.



Kwa upande wake Afisa Mradi unaowahusisha wanaume na wavulana kushiriki katika kuleta mabadiriko ya Kijinsia” Man engage”unaofadiliwa na shirika lisilo la Kiserikali la Care international Gega Bujeja alisema kuwa  baadhi ya ya kesi za ujauzito za wanafunzi nyingi zimekuwa zikiishia njiani hata kama ushahidi wa kutosha upo.



Bujeja aliendelea kusema kuwa pia kitu kingine kinachosababisha kesi hizo kusuasua ni pamoja na ushirikinao mdogo baina ya wazazi wa wanafunzi waliopewa  mimba  sambamba na waathirika wa suala hilo katika kutoa ushahidi wa kweli pindi wanapotakiwa mahakamani.



Hata hivyo Afisa huyo alisema kuwa kwa kupitia mradi huo wa MAN ENGAGE Shirika hilo litaanza kutoa Elimu kuhusu afya uzazi kwa wazazi katika maeneo mbalimbali wanapofanyia kazi katika kata za Bugarama, Bulyanhulu  na  Lunguya  hali ambayo inaweza kuleta mabadiliko katika siku za baadaye.



Katika kikao hicho kilichojumuisha Waandshi wa habari, Mtendaji wa kata ya Bugarama pamoja na Mratibu Elimu kata wa kata hiyo kilikuwa na lengo la kutafuta ufumbuzi wa Mwanafuzi huyo aliyepatiwa ujauzito mwaka jana na Masanja Julius Mkazi wa Igwamanoni na hivyo kesi hiyo kuonekana kusuasua hali ambayo ilimfanya Mkuu huyo wa Wilaya kutoa maagizo kwa jeshi la Polisi kutafuta majalada ya kesi hiyo ili yaweze kupitiwa upya.




KUONA VIDEO MPYA BOFYA HAPA CHINI