Saturday, September 27, 2014

MESSI,BARCELONA WAKIONA CHA MOTO

BOFYA HAPA CHINI KUONA MAAJABU YA LEO



BEKI wa kati wa Malaga,Welgton amedai aliitwa mtoto wa Kahaba na mshambuliaji,Lionel Messi hiyo ndio sababu
ya kumshika mdomo wake na kumsukuma chini.








Kikosi cha Malaga kinachonolewa na Javi Gracia,kilikuwa cha kwanza katika msimu wa 2014 – 15 kuwadhibiti Barcelona kiasi cha kutoshana nguvu,na washindi wa pili wa La Liga kushindwa kupiga hata shuti moja langoni mwa Maliga.



 Katika mchezo huo ghafla Weligton alionekana kumshika mdomo Messi,ambaye alianguka na wachezaji wa Barca kumshawishi mwamuzi amtoe nyota huyo raia wa nchini Brazil kwa kadi nyekundu,lakini alionyeshwa kadi ya njano.


  
Akizungumza na mtandao wa Cope,baada ya pambano hilo Weligton alidai alichukua maamuzi hayo kutokana na kutukanwa na Messi,ambaye katika mchezo huo hakufurukuta kutokana na kudhibitiwa ipasavyo na Mbrazil huyo.

Kocha wa vijana wa Barca,Luis Enrique alikiri vijana wa Malaga kuwazidi akili viungo wake kiasi cha kushindwa kumchezesha ipasavyo Messi ambaye mara nyingi huwa mkuki mchungu wa timu wanazokutana nazo.


Kocha huyo alikiri kumficha Messi kuliua makali ya timu yake ambayo ilikosa uelekeo kiasi cha kumaliza dakika tisini pasipo kupiga hata shuti moja langoni kwa wapinzani wao.


KUONA VIDEO MPYA BOFYA HAPA CHINI