Wednesday, September 17, 2014

WANAUME KAHAMA WAASWA KUONDOKANA NA MALEZI YA MFUMO DUME

BOFYA HAPA CHINI KUONA MAAJABU YA LEO


MWANDISHI wa habari kutoka Kahama FM Bakari Khalid  akiwasilisha majibu yaliyotokana hoja iliyotolewa na Mwezeshaji Emma Mashobe.
 
WANAUME  wilayani Kahama katika mkoa wa Shinyanga wameaswa kubadilika katika mtazamo chanya juu ya malezi ndani ya familia zao ili kuweza kuondokana na mfumodume  unaowakandamiza wanawake na watoto hali ambayo imeonyesha
kuwepo kwa ongezeko la ndoa za utotoni.


MWANDISHI wa habari wa magazeti ya Mwananchi,Mwanaspoti na The Citizen Mkoani Shinyanga Shija Felician,akichangia mada katika semina ya siku tatu inayotolewa na Care International wanaotekeleza Mradi wa Wanaume na Wavulana katika kuleta Mabadiriko ya Kijinsia.

Hayo yalielezwa na Meneja wa mradi wa Wanaume na Wavulana katika kuleta Mabadiriko ya Kijinsia "Men-engage"  Emma Mashobe kutoka shirika lisilo la kiserikali la Care- International  katika semina ya siku tatu inayoshirikisha waandishi wa habari 15 kutoka Mkoani Shinyanga inayofanyika mjini Kahama.

  
 Wandishi wa Habari wakimsikiliza mwezeshaji katika mafunzo hayo 
 
Mashobe alisema mradi huo ulioanza mwaka 2012 unatarajia kufikia ukomo Desemba mwaka huu ambapo mpaka sasa wamefanikiwa kupata mawakala wa mabadiriko 575 ambao ni wanaume na wavulana.

WAANDISHI wa habari  wakiwa katika semina wilayani Kahama  mkoani Shinyanga iliyoandaliwa na shirika lisilo la kiserikali la Care International Tanzania.
Alifafanua miongoni mwa mawakala hao 250 ni vijana wa kiume kutoka Shule za Msingi na Sekondari katika Kata za Lunguya,Bugarama na Bulyanhulu zilizo Halmashauri ya Msalala wilayani Kahama huku akibainisha lengo la mradi ni kutaka mabadiliko ya usawa wa kijinsia kati mwanaume na mwanamke.


WAANDISHI  wa habari  wakiwa  katika maelekezo ya vitendo.
Mashobe amewaeleza waandishi wa habari kuwa mradi huo tangu kuanza kwake umeweza kuleta mabadiliko kwenye baadhi ya familia na kupunguza ndoa za utotoni  ambapo ndani ya wilaya ya Kahama zililengwa kata tatu za Lunguya,Bugar ama na  Bulyanhulu na  lengo ni kuwafikia wasichana 8000.


WAANDISHI wa habari wakiwa katika mjadala wa vitendo.
Aidha alisema Wanaume wamepewa kipaumbele kwenye mafunzo hayo kutokana  na kuhusika kwa asilimia kubwa  kwakufanya vitendo  vya mfumo dume hivyo wameona watoe elimu ili waweze kubadilika sambamba na mafunzo hayo kutolewa kwa waandishi wa habari ili waweze kufikisha ujumbe.
Pia  kwa upande wa vijana wamekuwa  wakitoa elimu mashuleni  kupitia vilabu vyao vilivyoundwa  ikiwemo  vikundi vya burudani kufikisha ujumbe  kwa wenzao.


MWANDISHI wa habari   wa magazeti ya Habarileo na Dailynews mkoani Shinyanga  Raymond Mihayo akichangia Mada.
Hata hivyo Mwandishi wa habari  wa magazeti ya habarileo Raymond  Mihayo amesema kuwa  mashirika mengi  yamekuwa yakijikita  katika halmshauri ya wilaya ya                Msalala  zaidi ambapo  hata katika halmashauri ya Ushetu bado kunachangamoto nyingi za unyanyasaji wa kijinsia kwa watoto wa kike.















KUONA VIDEO MPYA BOFYA HAPA CHINI