![]() | |||||
EMANUEL Okwi akipongezwa na wachezaji wenzake baada ya kufunga bao |
halijapatiwa tiba msimu huu,baada ya mara ya pili mfululizo kushindwa kuutumia vyema uwanja wake wa nyumbani,kwa kulazimishwa sare ya bao 1 – 1 na maafande wa Polisi Moro.
![]() |
KIPA Abdul Ibad akichupa bila mafanikio kuokoa shuti lililozaa goli la kwanza,lililofungwa na Emmanuel Okwi. |
![]() |
MSHAMBULIAJI Dan Mrwanda wa Polisi Moro akipongezwa na wenzake baada ya kuisawazishia timu yake bao. |
Mnamo
dakika 50 Danny David Mrwanda alifunga goli la kusawazisha baada ya mabeki
wawili wa Simba, Masoud Nassor ‘Cholo’ na nahodha Joseph Owino kugongana na
kumuacha nyota huyo wa zamani wa Simba akifunga.
Kabla
ya mechi hiyo, Septemba 20 mwaka huu, Mnyama aliambulia sare ya 2-2 dhidi ya
Coastal Union katika mechi ya ufunguzi wa ligi kuu uwanja huo huo wa Taifa.
Simba
walianza mechi kwa kutawala safu ya kiungo ambapo Jonas Mkude alionesha kiwango
kizuri. Alitawala dimba la kati, alikuwa na jeuri, alipiga pasi sahihi na
kuipandisha timu juu, lakini mambo yalibadilika kipindi cha pili.
Mkude
alionekana kuchoka, wakati huo huo Piere Kwizera, Shaaban Kisiga, Emmanuel Okwi
waliokuwa mbele yake walishindwa kurudi nyuma ipasavyo na kuisaidia timu.
Aidha
katika uwanja wa Azam Complex uliopo Chamazi jijini Dar Es Salaam bao mbili
zilizowekwa kimiani kila kipindi na Didier Kavumbagu yaliiwezesha timu ya Azam
kuibuka na ushindi wa bao 2 – 0 dhidi ya maafande wa Ruvu Shooting.
Nao
vijana wa Stendi United kutoka mkoani Shinyanga walizinduka usingizini baada ya
kuifunga Mgambo JKT katika uwanja wa Mkwakwani Tanga kwa bao 1 – 0.Na kwenye
uwanja wa Manungu Turiani Morogoro Mtibwa waliendeleza wimbi la ushindi kwa
kuibabajua Ndanda FC kwa bao 3 – 1.
KUONA VIDEO MPYA BOFYA HAPA CHINI