MKUU wa wilaya ya Kahama Benson Mpesya akiongea na Wahitimu,wanafunzi,walimu na wazazi katika mahafari ya kumi ya Shule ya Sekondari ya Mhongolo Progressive. |
KATIKA kuboresha elimu nchini,Serikali imekumbushwa kutozisahau Shule za binafsi kuzipatiwa misaada ya vitabu kama inavyofanya katika shule inazozimiliki.
Rai hiyo ilitolewa na Mkuu wa Shule ya Sekondari ya Mhongolo Progressive ya wilayani Kahama,Jeremiah Gunda wakati wa mahafari ya kumi ya kidato cha nne mbele ya mkuu wa wilaya ya Kahama Benson Mpesya.
Mwalimu Gunda aliikumbusha serikali kuwa shule za binafsi ni wadau wakubwa katika sekta ya elimu nchini hivyo pindi inapopatikana fursa ya misaada ya vitabu vya kiada na ziada nazo zipatiwe kwa faida ya vijana wa Tanzania ambao wanasoma katika shule hizo za kulipia.
VIJANA walioghani shairi wakiwawakilisha wahitimu wenzao wakitoka kwa madaha ukumbini |
MKUU wa Shule ya Sekondari ya Mhongolo Progressive,Jeremiah Gunda akisoma risala. |
MKUU wa wilaya ya Kahama Benson Mpesya akitoa nasaha. |
Add caption |
MKUU wa wilaya akimpongeza mmoja wa wahitimu. |
Mbale alisema zawadi hizo zitachochea ushindani wa masomo kwa wanafunzi,hali itakayosaidia kunyanyua kiwango cha taaluma shuleni hapo na taifa kwa ujumla.
WANAFUNZI wa kidato cha tatu wakiserebuka. |
Alisema katika kutekeleza utaratibu huo,kwa mwaka huu shule imetenga kiasi cha Shilingi 1,950,000/= zilizokabidhiwa kwa wanafunzi Ishirini na Sita wa kidato cha tatu,waliopatiwa Shilingi Elfu Hamsini kila mmoja.
Alisema wengine walionufaika na utaratibu huo kwa mwaka huu ni wanafunzi Kumi na sita wa kidato cha pili waliopatiwa fedha taslimu Shilingi Elfu Tano kila mmoja.. .
WAHITIMU wa kidato cha Nne wakiserebuka |
Wahitimu katika sekondari hiyo wanaotarajia kuanza mitihani yao ya kumaliza kidato cha nne,walikuwa wanafunzi sitini na tisa,huku wasichana wakiwa Ishirini na Sita na Arobaini na tatu ya watoto wa kiume.
WAHITIMU wa kidato cha nne wakiimba kwa bashasha |
WAHITIMU wa kidato cha Nne. |
KUONA VIDEO MPYA BOFYA HAPA CHINI