Tuesday, February 27, 2018

UVAMIZI WA UJENZI ENEO LA CHUO WAPIGWA “STOP”

BOFYA HAPA CHINI KUONA MAAJABU YA LEO


AMRI imetolewa ya kusitisha,ujenzi wa nyumba za makazi katika Mtaa wa Igomelo,Kata ya Malunga,Halmashauri ya Mji,wilaya ya Kahama,Mkoani Shinyanga,kutokana na baadhi ya wananchi kushutumiwa kupoka Ardhi.


Uendelevu wa majengo katika eneo hilo,umepigwa marufuku,kufuatia kuvamiwa na kufanyika  shughuli za ujenzi, eneo la chuo cha Maendeleo ya Wananchi(MWAMVA).


Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Mkazi, William Lukuvi, jana alichukua maamuzi hayo chuoni hapo katika Mkutano wa hadhara, baada ya kupokea malalamiko kutoka kwa Kaimu Mkuu wa chuo cha Mwanva,Wamoja Matanza, kuwa sehemu ya eneo la chuo hicho,limevamiwa na kujengwa nyumba za makazi.


Matanza alisema Chuo hicho kilichoanzishwa mwaka 1978,mnamo mwaka 1977 kilipewa hekari 340,na serikali ya kijiji kwa ajili ya shughuli za ufugaji na kilimo ,lakini zimebaki hekari sita baada ya kuvamiwa na wananchi wanaojenga nyumba za makazi.


Aliitupia lawama Halmashauri ya Mji wa Kahama,kukuza mgogoro huo baada ya kushindwa kulipima eneo hilo,licha ya Chuo hicho cha Mwanva,kufuata utaratibu na kulipia  gharama za upimaji Shilingi Milioni Mbili.


 “.. baada ya kupeleka maombi hayo Halmashauri ilipima hekari 48, zilizokataliwa na aliyekuwa mkuu wa chuo hicho miaka ya nyuma, kwakuwa zilikuwa chache na ilivyokuwa hapo awali,ndipo wananchi walipovamia kujenga nyumba za makazi kiholela,”alisema.  


Kufuatia malalamiko hayo Waziri wa ardhi Nyumba na Maendeleo ya makazi William Lukuvi aliamuru wananchi kusitisha ujenzi katika eneo hilo hadi hapo atakapounda tume ya uchunguzi ni namna gani wananchi walipatiwa eneo hilo,linalodaiwa mali ya Chuo cha  MWAMVA .


Lukuvi alisema kuwa Ofa na hati zilizotolewa na Halmashauri hazipo kihalali kwani kuna baadhi ya hati na ofa hazikulipiwa na nyingine zikionesha kugushiwa nakuongeza kuwa kugushi nyaraka ya serikali kwa kujipatia eneo nikosa kisheria na hao waliogushi ofa na hati wataisaidia tume ni namna gani walipata maeneo hayo.


Kwa upande wake Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Kahama, Anderson Msumba, alisema hati na ofa zilizotolewa kwa wananchi waliovamia eneo la Mwamva ni batili na kuongeza zilitolewa na Afisa ardhi mteule,aliyefukuzwa; Charles Kitalya,  kipindi cha Halmashauri ya wilaya ya Kahama.


“Mheshimiwa Waziri hati na Ofa unazoziona hapa Halmashauri yangu haihusiki nazo nawala haizitambui   zilitolewa na halmashauri ya wilaya kabla haijagawanyika na kupatikana halmashauri za Mji,Msalala na Ushetu,mbali na hivyo, niliisitisha ujenzi na utoaji wa ofa ama hati katika eneo hili” alisema Msumba.


Nae Mwenyekiti wa Mtaa wa Igomelo kata ya Malunga wilayani hapa Agustino Mabula alisema kuwa eneo la Chuo cha Maendeleo ya Wananchi,kabla ya kupewa chuo hicho lilikuwa likimilikiwa na  kijiji nakuongeza kijiji ndio kilikuwa kikigawa maeneo hayo kwa wananchi waliotaka kujenga katika eneo hilo hali iliyopelekea wananchi kujenga makazi na wengine kuuza.


Hoja hiyo ya mwenyekiti ilipingwa na Waziri Lukuvi kwa madai kijiji hakina mamlaka ya kugawa ardhi ya serikali,isipokuwa serikali ya Mtaa kwa makubaliano na wananchi baada ya kuitisha  vikao malumu na kuandika mihutasari na kusisitiza kuwa wananchi waliojenga kwenye eneo hilo walijenga kimakosa.


Aidha Lukuvi alisema  hati na ofa ni nyaraka muhimu sana ya serikali, kama pasipoti ya kusafiria na haigushiwi na mtu yoyote na kwa aina yoyote ile,na kuonya  kwa   waliogushi kujipatia maeneo kinyume na utaratibu wataisaida tume katika kutatua mgogoro baina ya chuo hicho na wananchi wanaozunguka chuo.


KUONA VIDEO MPYA BOFYA HAPA CHINI