Saturday, February 24, 2018

UKAGUZI WA MAGARI KUANZA MACHI MOSI,MWAKA HUU.

BOFYA HAPA CHINI KUONA MAAJABU YA LEO

M
ACHI Mosi mwaka huu,utaanza ukaguzi wa magari binafsi kwa nchi nzima,huku ikilazimika kwa gari litakalokamilisha ukaguzi kulazimika
kulipia Shilingi elfu tatu kasha kupatiwa Stika ya uthibitisho.

Kufuatia kuanza kwa zoezi hilo Mwezi ujao,Wamiliki wa magari madogo watatakiwa kupeleka gari zao,katika vituo vya polisi vilivyo karibu na makazi ama maeneo yao ya shughuli zao,kusudi yafanyiwe ukaguzi kama yanastahiki kuendelea kuwepo barabarani.

Naibu Waziri wa Mambo ya ndani,Masauni amewaeleza  hayo jana mbele ya Wanahabari, huku akiwaasa askari wa barabarani kutekeleza majukumu yao kwa ueledi mkubwa .

Amesema , "Askari yoyote atakayetumia nafasi yake kutoa stika ya gari bila kulifanyia ukaguzi na ilihali halina vigezo vya kupewa stika nataka niwaambie kuwa huu si wakati wake, zama zimebadilika".

Pamoja na hayo Mh. Masauni aliongeza kwamba "Nataka madereva  wa pikipiki ambazo zitakamatwa na kukutwa zimesajiliwa kwa majina ya kampuni badala ya majina binafsi wachukuliwe hatua mara moja".

Kwa upande wake Kamanda wa Kikosi cha Usalama Barabarani Tanzania, Fortunatus Musilimu alisema katika Ukaguzi wa magari madogo utakaoanza mwezi ujao, mtu atakaekiuka na kukataa kupeleka gari lake kufanyiwa ukaguzi atakamatwa na sheria itachukua mkondo wake.


KUONA VIDEO MPYA BOFYA HAPA CHINI