Thursday, November 9, 2017

POLISI WAPATIWA ELIMU JUU YA WATOTO WA MITAANI

BOFYA HAPA CHINI KUONA MAAJABU YA LEO



J
eshi la Polisi sambamba na wadau kutoka sekta mbali mbali jijini Mwanza  wameelimishwa kubadilisha mitazamo
yao juu vijana wa mitaani,kuwa ni jamii isiyowezekana iliyotawaliwa na vitendo vya kiharifu.




Wameaswa kuondokana na fikra kwa   vijana wa mitaani kuwa ni jamii iliyoshindikana kimaadili na wanaokwaza jitihada za kujikwamua kimaisha kwa baadhi ya watu, badala yake wawaone kuwa wana mitazamo chanya ya kuleta maendeleo ya nchi,anaandika   Tunu Herman; Mwanza.

 Afisa Mradi wa Shirika la Railway Children Africa,Adamu Kaombwe,amesema jamii ina mtazamo hasi na vijana wa mitaani kiasi cha kuwakatia tamaa,kitendo ambacho si cha kiungwana,na kutokana na kubaini hilo shirika lake limeona ni vyema likaanzisha hamasa ya kuwathamini vijana hao.

Amesema kuokana na jamii kutowathamini vijana shirika lake likaamua kuwakutanisha wadau kutoka sekta mbalimbali ikiwemo Jeshi la Polisi kwa lengo  kuzungumzia changamoto zinazowakabili watoto wa mitaani ambazo zimekuwa  chanzo cha wao kutokukubalika katika jamii.

Alisema kwa sasa, jamii imewatenga kutokana na muonekano wao wa nje pasipo kujua ndani wanamalengo mazuri, hivyo wakati umefika wa kuwathamini na kushirikiana nao katika fursa mbalimbali zinazojitokeza.

“ Matumaini yangu  ni kuwa kupitia  semina hii, kila mtu atakuwa na muonekano mpya na kuondoa daraja lililopo mbele la utengano  na kuweka umoja utakaoleta tija na maendeleo ya nchi “alisema Kaombwe.

Kwa upande wake Afisa Ustawi wa Jamii mkoa wa Mwanza Wambura Kizito alisema, ili kuleta usawa kati ya jamii na vijana hao, ni vyema yakahamasishwa mabadiliko  kuanzia muonekano wao wa uvaaji,ili uwe wa staha.

Wambura amesema pia kuwahamasisha vijana hao, kushiriki shughuli za kijamii pamoja na kuanzisha vikundi ambavyo vinatambuliwa   na serikali  ili  waweze kupata mikopo pamoja na wale wenye watoto kuhakikisha  hawaingii mitaani.

Naye Prisca William mmoja ya watoto waliokuwa wanaishi mitaani  alisema wataitumia vizuri fursa hiyo walioipata ya kukutanishwa na viongozi wa polisi na wadau kwani mwanga uliopotea kwa muda mrefu umeanza kuonekana ambapo mwanzo walikuwa wanaona kila mtu anayewazunguka ni adui kwao.

Alisema jamii itambue sasa nao wanajitambua, wanajiamini na wana uwezo wa kufanya vitu ambavyo vinaweza kukubalika na kuleta maendeleo hivyo washirikishwe kwa kila fursa zinazojitokeza .

Hata hivyo Mkuu wa Polisi wa wilaya ya Ilemela  SSP Ndagile Makubi  alisema, wanahitaji Tanzania inayosaidia jamii na vijana wanaozingatia maadili na kutii sheria na kuacha tabia ambazo siyo nzuri,kuepuka makundi mabaya, kushinda vijiweni na sehemu zinazotiliwa mashaka sambamba na kufanya kazi halali.

Pia aliwaomba vijana hao kushirikiana na jeshi la polisi kwa kutoa taarifa za uhalifu, ili kuhakikisha tunakuwa na taifa salama na lenye amani.

KUONA VIDEO MPYA BOFYA HAPA CHINI