Thursday, November 9, 2017

CHAMA CHA WALIMU SHINYANGA CHAVUNJWA.

BOFYA HAPA CHINI KUONA MAAJABU YA LEO




M
uasisi wa Chama cha Kutetea Haki na Maslahi ya Walimu Tanzania ( CHAKAMWATA ),Mkoani Shinyanga,Mwalimu Lawrance Mbaga,ameuvunja uongozi wa chama hicho baada ya
kubaini hakijajikita kutetea maslahi ya walimu na kurejea chama chake cha zamani cha CWT.




 Mbaga ambaye alikuwa Katibu wa CHAKAMWATA,Mkoa wa Shinyanga,pia akitumikia wadhifa huo ngazi ya wilaya ya Kahama,aliuvunja  uongozi na kukabidhi nyaraka zote za chama hicho kwa uongozi  wa Chama cha walimu (CWT ) wa wilaya ya Kahama,katika kikao kilichofanyika katika ofisi za CWT wilayani Kahama.

Alisema kisheria ana nguvu ya kuvunja uongozi huo kwakuwa ndiye aliyeuteua tena kwa kuzingatia urafiki,pasipo kuzingatia kikao ama mkutano wowote na kuwapangia mamlaka ya kuongoza kwa nyadhifa zile zile kuanzia ngazi ya wilaya hadi Mkoa.

Mbaga ambae ni mwalimu wa Shule ya Msingi Masabi katika Halmashauri ya Msalala wilaya ya Kahama alisema ameamua kuvunja uongozi huo,baada ya kubaini uwepo wake umekuwa sababu ya kuwagawa na kuvunja umoja na mshikamano katika kutetea maslahi ya walimu pamoja na kutatua changamoto zinazowakabili.

Alidai kubaini CHAKAMWATA hakipo kwa ajili ya kutetea maslahi ya walimu bali ni  kupinga chama kilichopo cha CWT ambacho kina malengo sahihi kwa walimu huku kikiwa kimeishafanya mambo mengi mazuri yenye kutatua changamoto zinazowakabili katika majukumu yao.

“CHAKAMWATA walinirubuni nilipokuwa likizo nyumbani Mbeya,viongozi wa chama hicho wana tatizo la ueneo,kutokea kwangu Mbeya ndiyo ilikuwa sifa ya kupata nafasi hiyo,ntahakikisha wanachama wachache niliowalaghai ninawarejesha CWT,”alisema Mwalimu Mbaga.

Aidha alitumia fursa hiyo kuwaasa walimu wenzake kutohadaika na kuanzisha vyama vingine vinavyokinzana na CWT,ambavyo vinakuwa sababu ya migongano isiyo na tija katika umoja na mshikamano wao ambao ndio silaha kubwa ya kutetea maslahi yao.

“Mshikamano ndiyo ukombozi wa wafanyakazi kitendo cha kuanzisha chama kingine cha walimu ni kuwagawa na kumomonyoa nguvu na mshikamano wa walimu ndiyo maana tumeamua kuivunja CHAKAMWATA na kurudi CWT ,, Alisema Mbaga.
  
Mwenyekiti wa CWT wa wilaya ya Kahama ,Edina Kalambo,alipongeza maamuzi ya muasisi wa CHAKAMWATA wilayani Kahama na mkoani Shinyanga, kujiondoa katika chama hicho, kwa sababu kilichopo cha CWT kipo imara katika kutatua changamoto za walimu zinazowakabili.

Mwalimu Kalambo aliwakumbusha kwamba CWT ipo kwa ajili ya kutetea maslahi mapana ya walimu na kuwataka kuacha kugawanyika bali waendeleze umoja wao na mshikamano hatua itakayowasaidia kuwafikisha mbali ya kiuchumi na taaluma yao.

Nae Katibu wa CWT wa wilaya ya Kahama Dauda Mohammed Bilikesi,alionya tabia ya kuanzisha utitiri wa vyama,ambavyo vinaweza kuwa sababu kudhoofisha nguvu ya CWT ambacho hata hivyo alijinasibu kuwa kipo   imara na kinawajibika ipasavyo kutetea stahiki za walimu.

Kwa upande wake mwenyekiti wa CWT wa mkoa wa Shinyanaga George Nyagusu alisema viongozi walioanzisha chama hicho kipya cha CHAKAMWATA ambacho makao yake makuu yapo mkoa wa Mbeya na walioanzisha ni baada ya kukosa nafasi za uongozi katika chaguzi za CWT za taifa.

Alitoa wito kwa walimu kujiunga na chama chao cha CWT kwa sababu kipo imala , kutetea maslahi yao na kuwataka wasigawanyike na kuendekeza kuanzisha vyama vipya na kuwaomba walimu wote nchini kutimiza wajibu wao kabla hawajadai stahiki zao.

 CHAKAMWATA kilianzishwa na kupata usajiri wake Machi 18 , 2015 kikiwa na Makao Makuu yake mkoani Mbeya na kilimteua Mbaga kuwa katibu wa mkoa wa Shinyanga na kuunda uongozi ambao kwa pamoja wameamua kujivua madaraka hayo na kurejea CWT.

KUONA VIDEO MPYA BOFYA HAPA CHINI