M
|
abingwa watetezi wa Ligi Kuu Tanzania
Bara,Yanga African na watani zao wa Jadi,Simba Sport Club,wanateremka dimbani
leo kumenyana kwenye mchezo wa Ngao ya Jamii,ambao ndio ufunguzi wa Msimu Mpya
wa Ligi Kuu mwaka 2017/2018.
Pambano
hilo la Watani wa Jadi,kwa historia ya timu hizo humalizika kwa timu
inayopoteza mchezo kutoyakubali matokeo kimchezo,kwa mkasa wa kutimua benchi la
ufundi pia kuibua hujuma kwa baadhi ya wachezaji ama viongozi wa timu.
Katika
pambano hilo la Ngao ya Jamii,litakalopigwa Uwanja wa Taifa,Dar Es Salaam,litakuwa hitimisho la tambo za
mashabiki wao,huku wale wa Simba wakionekana kuwanyong’onyesha wenzao
wakitambia usajili wao wanaodai umewapatia kikosi bora na kipana zaidi.
Ally
Yusuf “ Tigana” winga wa zamani aliyepata kuzichezea timu hizo kwa nyakati
tofauti,amenukuliwa na vyombo vya habari,akisema mchezo huo si mwepesi kutokana
na tabia za Klabu hizo,kwa kuwapa ujiko ama kuwatibulia makocha ,viongozi na
wachezaji.
Mdau
Mkubwa wa Soka Nchini na Mwalimu wa Soka,Imam Mabrouky,anasema pamoja na
changamoto zinazotokea kwa pambano la Watani wa Jadi,lakini kuna haja ya kuzama
zaidi katika kubadili mifumo ya timu hizo ambazo ndio dira ya soka la nchini,hatua
itakayosaidia kupata maendeleo ya mchezo wa soka.
Nae
Zamoyoni Mogella “Golden Boy”,mshambuliaji mahiri wa zamani wa timu hizo na
Taifa Stars,amesema mchezo wa watani wa jadi daima huwa haitabiriki,bali timu
yenye nidhamu ndio huibuka mshindi.
Ama
hakika pambano la timu hizo si rahisi kumtabiri mshindi,kwani mara nyingi huwa
na matokeo ya kushangaza,kwani huwa zaidi ya kuwa na kikosi bora kwa wakati
huo,uchumi mzuri uliosaidia usajili na maandalizi mazuri lakini matokeo yakawa
hasi.
Lakini
hayo ni tisa,kumi ni mikasa inayoibuka baada ya pambano la Watani wa Jadi,kwani
ada kutimua benchi la ufundi kwa timu inayofungwa,na pindi likisalimika basi
jumba bovu hilo huwaangukia baadhi ya wachezaji hata viongozi wakidaiwa
kuhujumu timu.
Katika
suala la kutimua benchi la Ufundi ndilo hupewa kipaumbele na viongozi wa timu
hizo kwa dhana ya kujisafisha kwa mashabiki wao na kumbukumbu zinaonesha Yanga
imepata kutimua benchi lake lote la Ufundi,lililokuwa chini ya Ernie Brandts na
Fred Felix “Minziro”.
Hii
baada ya matokeo ya pambano la 13 Desemba 2013,la Nani Mtani Jembe,lililopigwa
Uwanja wa Taifa na Wanajangwani kuambulia kichapo cha bao 3 – 1.
Pia
katika pambano hilo lilichezwa 13
Desemba 2014,halikuliacha salama Benchi la Ufundi la timu hiyo,lililokuwa likiongozwa
na Kocha Marcio Maximo baada ya kupokea kipigo cha bao 2 – 0 kutoka kwa Watani
zao hao,katika pambano lililopigwa pia Uwanja wa Taifa.
Simba
Sports Club nao kwa nyakati mbalimbali imepata kuwatimua Milovan
Circovic,Patrick Liewig,Patrick Phiri,Abdallah Kibadeni,Zdravko Logarusic,Goran
Kopunovic na Dylan Kerr.
Ni
utamaduni ambao hauna afya kwa soka letu nchini,lakini ndio imezoeleka kwa
Klabu hizo mbili kukubali kushindwa kwa stahili hiyo ya kuwatupia lawama
wachezaji kucheza chini ya kiwango,ama miongoni mwa viongozi kuhujumu mechi na
kubwa zaidi ni kufukuza makocha kila kukicha.
Sasa
katika pambano la leo,ni kiongozi ama viongozi pia wachezaji watakaoangukiwa na
jumba bovu hilo?Na benchi lipi la Ufundi litafumuliwa?Ni kocha Joseph Omog wa Simba?ama
George Lwandamina wa Yanga?Ama safari hii timu hizi zitabadilika kwa kuona
vitendo hivyo vimepitwa na wakati?Muda utaamua.
KUONA VIDEO MPYA BOFYA HAPA CHINI