K
atika
kuhakikisha inafikia malengo sahihi,Serikali imesema itaendelea kusimamia
utendaji kazi wa watumishi wa Halmashauri nchini, kuanzia ngazi ya Wilaya mkoa
hadi Taifa.
Naibu Waziri Ofisi ya
Rais Tawala za Mikoa na serikali za mitaa TAMISEMI Suleiman Jafo amesema hayo wakati
wa ziara yake ya kukagua miradi ya maendeleo katika Wilaya ya Kigamboni
iliyokwenda sambamba na mkutano Maalumu na viongozi pamoja na watumishi
wa Manispaa ya Kigamboni jijini Dar es Salaam.
Amesema utendaji kazi bora utakaofanywa na watumishi
wa Kigamboni pamoja na viongozi wao utaufanya Mji huo kuwa wenye
maendeleo ukilinganisha na maeneo mengine.
Miongoni mwa miradi ya Maendeleo ambayo Naibu Waziri Jafo ameyatembelea
ni Pamoja ujenzi wa mabweni kwaajili ya wanafunzi wa kidato cha tano na
cha sita wa Shule ya Sekondari Nguva.
Hospitali ya Wilaya ya Kigamboni
iliyopo vijibweni ambapo akiwa shule ya Sekondari nguvu Naibu Waziri
Jafo amewataka wanafunzi kuongeza bidii kwenye masomo ili wapate matokeo
mazuri kwenye mitihani ya Taifa.
Aidha amemuagiza Mkurugenzi wa Manispaa hiyo Stephen Katemba kukaana
menejimenti yake kuona namna ya kujenga duka kubwa la dawa litakalo
hudumia wanachama wa bima ya Afya ambao kwa sasa wanapata shida
kutokana na kila mara kuandika kujua dawa nje ya hospitali.
Kwa upande wake Mganga mkuu wa Manispaa hiyo Bakari Mbwana Amemwambia
Waziri Jafo kuwa upungufu wa Dawa unasababishwa na idadi kubwa ya
wanachi ukilinganisha na bajeti wanayo pewa ambapo kwa mujibu wa
bajeti hiyo ni wa tu Laki mbili tu ndo walitoa kuwa kuhudumia huku
kukutwa na wananchi Zaidi ya Laki tano wanaotegemea kupatiwa huduma
katika Hospital hiyo.
Kwa upande wake Mkurugenzi wa Manispaa ya Kigamboni ndg Stephen Katemba
alimhikikishia Waziri Jafo kuwa maagizo yote aliyoyatoa
atayafanyiakazi.