M
|
bwana Ally Samatta,ameikoa timu yake
ya KRC Genk,kupokea kipigo toka kwa timu ya Everton,baada ya
kuisawazishia bao
na kufanya pambano baina ya timu hizo kukamilika dakika Tisini kwa kufungana
bao 1 - 1.
Samatta ameandika
historia ya kuwa Mtanzania wa kwanza,kuweza kufunga bao dhidi ya timu ya
Everton ambayo inashiriki Ligi Kuu ya England baada ya kufanya hivyo
katika mchezo wa kirafiki akiwa ndani ya jezi ya KRC Genk.
Samatta ambaye amekabidhiwa jezi namba kumi hivi karibuni katika kikosi hicho, amefanikiwa kuifungia timu yake
hiyo bao katika dakika ya 55 katika mchezo uliomalizika kwa sare ya bao
1-1 dhidi ya Everton ambao walikuwa na staa wao, Wayne Rooney.
Bao la Samatta lilipatikana baada ya
kupigwa pasi zaidi ya saba kuanzia kwa kipa wa Genk hadi mpira
ulipomfikia Samatta ambaye alimalizia kwa kupiga shuti kali. Mchezo huo
uliochezwa Jumamosi hii nchini Ubelgiji ni maalum kwa ajili ya kujiandaa
na msimu wa 2017/18 kwa timu zote mbili.
Bao la Everton lilifungwa na Rooney katika dakika ya 45.
Samatta amekuwa na mwendelezo mzuri
katika mechi za maandalizi ambapo wiki iliyopita pia alifunga bao moja
katika sare ya mabao 3-3 ya timu yake dhidi ya Ajax ya Uholanzi.
KUONA VIDEO MPYA BOFYA HAPA CHINI