Sunday, July 2, 2017

RAIS MAGUFULI AWAPA "BIG UP" WATANZANIA

BOFYA HAPA CHINI KUONA MAAJABU YA LEO

 
R
ais John Magufuli amevutiwa kwa jinsi Watanzania walivyoingiwa na mwamko,wa kuchangia mapato ya
serikali yao kwa kujitokeza kwa wingi kulipa kodi za Majengo.

Amedai Watanzania wamehamasishana na kujitokeza kwa wingi,kulipia kodi ya majengo,yao pasipo kusukumwa jambo ambalo linastahili kupongezwa.

Akizungumza jana wakati akizindua rasmi maonyesho ya kimataifa ya Biashara ya Sabasaba, Rais amesema Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) ilipochukua jukumu la kukusanya kodi hiyo imewezesha wananchi kulipa kodi kwa amani.

“Walipochukua TRA, sasa waliwathaminishia kodi ambayo wananchi wanaweza kuilipa, ndiyo maana wakajitokeza kwa wingi. Haijapata kutokea wananchi wakataka kulipa kodi kwa kiasi kile, ni kwa sababu ilikuwa nafuu kwao,” amesema

Pia, Rais amewataka TRA kuendelea kukusanya kodi kwa njia ambazo ni rafiki kwa kuwa wananchi hawapendi kodi inayowaumiza bali kodi ambayo ni sahihi kwao. 


“Wananchi wanapenda kulipa kodi lakini iwe na manufaa kwao,” amesema Rais Magufuli.

KUONA VIDEO MPYA BOFYA HAPA CHINI