Wednesday, May 11, 2016

SNURA ALITESWA NA CHURA

BOFYA HAPA CHINI KUONA MAAJABU YA LEO



Na Rajab Rachi.

MSANII wa Mduara,Snura Moshi,ambae video yake ya wimbo Chura ilizua gumzo mitaani na kwenye mitandao yakijamii amekiri kuteswa na wimbo kabla ya kufungiwa.

Snura aliomba radhi kwa serikali na watu wote waliokwazwa nao,nakuahidi kutorudia tena kosa hilo kufuatia jamii kumtafsiri kuwa ni mhuni aliyekithiri kufuatia wimbo wake wa Chura.

Alisema hakuwa na dhamira mbaya ya kuipotosha jamii hata kufikia kumbeza na kueleza umempa funzo na kuahidi kuwa balozi kwa maadili kwa wasanii wengine.

Snura alisema wimbo huo kusimamishwa na serikali kwa kukiuka maadili sambamba na kutojisajiri Baraza la Sanaa la Taifa {Basata} lakini siku hiyo hiyo {Mei 4} aliyosimamishwa alikwenda kujisajiri na kukumbushwa taratibu zote hivyo yupo huru kufanya sanaa.

Amesema ataulekebisha wimbo huo na kuendelea kuutumia,Huu ni wimbo wapili kufungiwa ukitanguliwa na Umevurugwa ambao pia ulifungiwa

KUONA VIDEO MPYA BOFYA HAPA CHINI