Wednesday, April 27, 2016

TAKUKURU KAHAMA INACHUNGUZA JENGO LA SEKONDARI LILILOTELEKEZWA.

BOFYA HAPA CHINI KUONA MAAJABU YA LEO

TAASISI ya kuzuia na Kupamba na Rushwa(Takukuru)Mkoa Maalumu wa Kahama,inaifanyia uchunguzi miradi minne ya maendeleo wilayani Kahama,ukiwemo wa jengo la Utawala katika Shule ya Sekondari ya Nyihogo,lililotelekezwa kwa kipindi cha miaka saba.
 
Akiongea na Waandishi wa Habari Mjini hapa Kaimu Kamanda wa TAKUKURU Mkoa maalumu wa Kahama Owen Jasson alisema kuwa taasisi yake  imekagua jumla ya miradi  11 ya maendeleo Wilayani hapa ili kubaini kama taratibu za  manunuzi zilifuatwa  ikiwa ni pamoja na wazabuni waliopewa kazi hizo kwa lengo la kubaini  ikiukwaji wa taratibu na matumizi ya fedha.
 
Jasson Alisema kuwa  Pia walikagua miradi hiyo ili kujiridhisha na kuona maendeleo ya Mradi husika na pia kuona kama gharama ziliztumika katika kutekeleza miradi hiyo ilikuwa ni sahihi na zinaendana na kazi iliyofanyika hali ambayo itachangia katika kuziba mianya ya Rushwa iliyopo.
 
Aliitaja baadhi ya Miradi waliotembelea kuwa ni pamoja na Mradi wa Maji, mmoja, Sekta ya Elimu miradi mitano, Afya miradi miwili, Madini miradi mitatu, na kuongeza kuwa kwa upande wa Elimu mradi mmoja uliokaguliwa ulikuta umetelekezwa  kwa muda wa miaka saba  ambao ni wa jengo la Utawala la Shule ya sekondari ya Nyihogo.
 
Pamoja na mambo mengine Kaimu Kamanda huyo alisema kuwa pia taasisi yake hiyo kwa kipindi cha  mwezi January hadi March 2016, Vilabu vya wapinga Rushwa viwili vimeimarishwa kwa kuwakumbusha Wanafunzi juu ya wajibu wao katika mapambano dhidi ya Rushwa pamoja na kupokea Wanachama wapya.
 
Hata hivyo alisema kuwa jumla ya machapisho 245 yalisambazwa  kwa Wananchi na kuongeza kuwa semina mbalimbali pia zimefanyika  kwa kuhusisha Walimu  wa shule ya Sekondari  na Wanafunzi sambamba na vikundi mbalimbali vya wasanii  pamoja na makundi mbalimbali ya Dini.
 
Kuhusu Kesi Kaimu Kamanda huyo alisema kuwa kwa kipindi cha miezi mitatu ya Januari hadi marchi mwaka huu kulikuwa na jumla ya kesi sita  zilizokuwa zikiendeshwa Mahakamani  ambapo nne ni za kipindi cha nyuma  yaani kabla ya Januari 2016 na kuongeza kuwa kesi moja kati hizo ilitolewa hukumu mwezi februari mwaka huu na walishindwa kabla ya kukata rufaa kwa kuwa hawakuridhika na hukumu hiyo.
 
Katika suala la mazingira Kaimu Kamanada huyo alisema kuwa kazi iliofanyika ni kufanya utafiti kuhusiana na mianya ya Rushwa katika usimamizi  na ukaguzi wa usafi wa mazingira ,kuandaa kikao cha Wadau kitakachofanyika mwezi aprili mwaka huu  kitakachowahusisha baadhi ya Watendaji wa kata, baadhi ya maafisa Afya kata, Mkuu wa idara ya afya Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji  pamoja na Maafisa wa TAKUKURU.
 

KUONA VIDEO MPYA BOFYA HAPA CHINI