Wednesday, April 27, 2016

LEMBELI:- NIPO TAYARI KUMUELEKEZA JPM MAJIPU YA KAHAMA.

BOFYA HAPA CHINI KUONA MAAJABU YA LEO

MBUNGE wa zamani wa Jimbo la Kahama,James Lembeli,amesema anamsubiri kwa hamu Rais wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania,John Pombe Magufuli,ili kumuelekeza yalipo majipu katika Halmashauri za Mji wa Kahama na ile ya wilaya ya Ushetu,ambapo amekiri kuwepo kwa ubadhirifu mkubwa wa mali za umma.

Akiongea katika mkutano mkubwa wa hadhara uliojumuisha wabunge;Salome Makamba wa Viti Maalum(Chadema)na Wilfred Rwakatare(Chadema) Jimbo la Bukoba Mjini pamoja na Mwenyekiti wa BAVICHA;Patrobas Katambi,Lembeli alisema pamoja na kwamba yupo upinzani lakini yupo tayari kumuelekeza Rais Magufuli majipu yanayoitafuna Kahama.


“Sina tatizo na CCM,bali tatizo langu ni watu wanaochaguliwa ndani ya CCM,watu hawa ni hatari kwasababu wanatumia fedha nyingi kuingia madarakani,lakini wanachoenda kufanya si kutetea maslahi ya wananchi,kwakuwa Halmashauri za Ushetu na Mji nazifahamu,namsubiri kwa hamu Magufuli nije nimuonyeshe Majipu na Vijipu uchungu atumbue,”alisema Lembeli huku akishangiliwa na umati wa watu.

MAKAMANDA wa CHADEMA katika Mkutano.
Lembeli ambaye uchaguzi uliopita aligombea Jimbo jipya la Kahama mjini na kushindwa,alisema hatua ambazo anazifanya Rais Magufuli,alidai walizifanya kwa kipindi cha miaka kumi ya Ubunge wake japokuwa serikali iliyokuwa madarakani ilionesha kupuuza harakati hizo.
Hata hivyo Lembeli alionesha mashaka ya kufanikiwa jitihada za Rais Magufuli kutokana na watu wanaomzunguka kutokuwa waadilifu na hivyo kumuomba apate maelekezo ya kuendelea kuwabaini wabadhirifu na mafisadi kutoka kwa watu ambao wapo nje ya CCM.
Katika hali isiyo ya kawaida baada ya kupanda jukwaani kwa viongozi hao wa Chadema ilishuka mvua kubwa ya ghafla,lakini wananchi hawakuweza kutawanyika bali walikuwa wakiimba Lembeli…Lembeli…Lembeli…Lembeli,hali iliyopelekea kukolea kwa shangwe hizo ni baada ya Mwenyekiti wa Bavicha Taifa,Katambi kushuka jukwaani na kuungana na umati huo kuimba na kucheza.
Kwa upande wake Mbunge wa Viti Maalumu,Salome Makamba,alishangazwa na kauli iliyotolewa na Mbunge wa Jimbo la Kahama,Jumanne Kishimba,kuwaita Madiwani na Watendaji wa Halmashauri kuwa ni Vimbulu,hawajitambui,wasiojua chochote kwa kushindwa kusimamia Halmashauri.
Makamba alisema kauli hiyo hakupaswa kuisema kwani inachochea chuki na kusababisha mgawanyiko huku ukikosesha ari ya watendaji wa halmashauri hatua aliyodai inaweza kusababisha kukosekana kwa maendeleo katika Halmashauri ya Mji,huku akiwataka Watendaji wa halmashauri hiyo kutimiza wajibu wao kwa waledi na kwa kuzingatia utaalamu waliosomea.

“Nimeshangazwa na kauli za Mbunge Kishimba,ni kauli zilizopaswa kutolewa na mtu ambaye hakusoma shule,nina mashaka na elimu yake,atambue kutembea sana sio kujua uhandisi na mambo mengine ya kitaaluma,mimi nina imani na Watendaji wa halmashauri naomba chapeni kazi,”alisema Salome.
Naye Mbunge wa Bukoba Mjini,Rwakatare,alionesha wasiwasi wake katika wizara ya ujenzi iliyokuwa ikiongozwa na waziri wa kipindi hicho ambaye ni Raisi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,kwa kuchelewa kutumbua majipu katika wizara hiyo ambapo alisema alisema zilitolewa Bilioni 889 katika Bajeti ya 2015/2016,lakini ameshangazwa na kitendo kilichofanyika Machi 2016 kwa kupeleka Bilioni 610 badala ya Bilioni 161 bila Bunge kupewa taarifa.
“Nina wasiwasi wa uhamishwaji wa fedha hizo bila ushiriki wa Bunge,inawezekana zimepekwa kufuidia madeni ya uchaguzi,kwani haileti picha nzuri kuhamisha kiasi kikubwa cha fedha pasipo kuwashirikisha wabunge,nimuombe CAG akague na kufanya uchunguzi juu ya uhamishwaji wa fedha hizo ili kubaini uhalali wa kuhamishwa kwa fedha hizo.”alisema Rwakatare.
 CHANZO cha Habari;-  Ali Lityawi na Antony Sollo.

KUONA VIDEO MPYA BOFYA HAPA CHINI