Monday, April 18, 2016

RAIS MAGUFULI AIBUKA NA LINGINE DAR,AWASHANGAZA WATANZANIA

BOFYA HAPA CHINI KUONA MAAJABU YA LEO

2m  
RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Dkt.John Pombe Magufuli,jana ameibuka katika staili ingine baada ya kuvamia tawi la Benki ya CRDB (Holland Branch),la Jijini Dar Es Salaam,akiwa kwenye gari lenye namba za usajili;T 182 DFQ huku likiwa halina nembo ya “Adamu na Hawa” wala bendera ya Rais,kitendo ambacho kimesababisha kuzusha mjadala.

Rais Magufuli alifanya kitendo hicho kisichotarajiwa,katika Tawi la benki hiyo ambayo ipo makutano ya barabara za Ohio na Samora, katika Tukio hilo lililochukuwa dakika 25,ambalo limetokea majira ya asubuhi jijijni Dar es Salaam.

Mara baada ya Rais Magufuli kufika katika eneo liliko tawi hilo, makutano ya barabara hizo yalifungwa ndipo Rais aliposhuka kwenye gari na kuingia ndani ya benki hiyo.

3m3
Rais Dk. Magufuli akipunga mkono  alipokuwa akiondoka 
Wakati akikaribia kuingia ndani ilibidi baadhi ya wateja waliyokuwa wakijiandaa kuingia ndani ya benki hiyoi wazuiwe kuingia huku huduma ikiendelea tu kwa wale ambao waliyokwishaingia.

Aidha, baada ya kuingia ndani baadhi ya wateja wa tawi hilo na wananchi wengine walibaki wakishangaa huku wengine wakijiuliza imekuwaje Rais kuingia benki kwa sitaili ile. Baadhi ya wananchi walisema hawajaona tukio kama lile kwa Marais wote waliyopita.

James Charles, ambaye ni dereva wa taxi, alisema baadhi ya wananchi waliyokuwa kwenye eneo hilo baada ya kuona ulinzi unaimarishwa walishituka na mara wakamuona Rais Magufuli akishuka kwenye gari, hali iliyowafanya wafikirie anakwenda kutembelea ofisi yake ya zamani.

“Lakini kufumba na kufumbua tukamuona anaelekea kwenye benki ya CRDB, tukajiuliza vipi rais leo kaamua kuwa kama mteja? Hata hivyo tujui kama hiyo ilikuwa inawezekana. Lazima kutakuwa na kitu. Haiwezekani aende akachukue fedha kwa utaratibu ule. Ngoja tusubiri tutasikia amefuata nini,”alisema Charles.

Joyce Godwin ambaye ni mwanafunzi wa chuo kimojawapo cha elimu ya juu alisema kuja kwake kumewashtua wafanyakazi wa tawi la benki hiyo kwani walidhani alikwenda pale kwa ajili ya kutumbua majipu.

“Mimi wakati Rais Magufuli anaingia nilikuwepo ndani kwenye foleni nikisubiri huduma. Kwa ujumla kila mmoja wetu alishituka lakini hatukujua kilichomleta,” alisema.

Baada ya Rais Magufuli kumaliza kazi yake iliyompeleka alitoka na kuingia kwenye gari huku akiwapungia mkono wananchi.

KUONA VIDEO MPYA BOFYA HAPA CHINI