Monday, April 18, 2016

MNYIKA AMUIBUKIA RAIS MAGUFULI

BOFYA HAPA CHINI KUONA MAAJABU YA LEO




 BAADA ya kimya cha muda mrefu,Mbunge wa Jimbo la Kibamba,jijini Dar Es Salaam,John Mnyika,ameibuka na kumtaka Rais John Magufuli,ahuishe Mchakato wa Katiba Mpya kwa kurejesha maoni ya wananchi.

Mnyika anasema,Rais Magufuli,anapaswa kuyafanyia kazi maoni ya wananchi yaliyokusanywa na aliyekuwa Mwenyekiti wa Tume ya Katiba, Jaji Mstaafu, Joseph Warioba,na si kubeba maoni yaliyotolewa na Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Anasema kuwa, Rais Magufuli anapaswa kujua kwamba, ni jambo la msingi na busara kuheshimu maoni ya wananchi kwa kuwa wao ndio wanaopaswa kuamua hatma ya taifa lao.

Awali Mnyika aliitoa kauli hiyo siku mbili zilizopita wakati wa uzinduzi wa Umoja wa Wanasheria -Justice Voices Tanzania (JVT) unaoshirikiana na Shirika la Maendeleo la Kimataifa (UDI).

Kwenye uzinduzi huo Mnyika amemtaka Rais Magufuli na Harrison Mwakyembe, Waziri wa Katiba na Sheria kutangaza siku ambayo Mchakato wa Katiba Mpya utaanza na kwamba, irejeshe rasimu ya Jaji Warioba.

KUONA VIDEO MPYA BOFYA HAPA CHINI