WAZIRI
wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo,Nape Nnauye amekifunga mara moja kiwanda
kilicho kuwa kikiendeshwa kwa njia zisizo halali na Wakandarasi wa Uwanja wa
Taifa, Kampuni ya Beijing Construction Engineering Group (BCEG) kutoka nchini
China.
Kutokana
na kusitishwa kwa karakana hiyo kumeifanya hatima ya Meneja wa Uwanja wa Taifa,Rish
Urio kuwa shakani,kunakosababishwa na mazingira ya uwepo kwa karakana hiyo.
Nape
alifanya zoezi hilo jana baada ya kufanya ziara ya kukagua maendeleo ya Uwanja wa
Uhuru “Shamba la Bibi” na kubaini kuwepo kwa kiwanda hicho ambacho ni kinyume
na taratibu na mkataba wa kisheria walioingia baina ya Serikali na Kampuni hiyo
ya Wachina kuhusu ujenzi wa miudombinu ya michezo pekee ikiwemo Uwanja wa Taifa
na Uhuru.
Kabla
ya kukifungia kiwanda hicho Waziri Nape aliomba maelezo ya kina juu ya uhalali
wa uwepo wake na namna uendeshwaji wake unavyofanyika ili kujiridhisha ndipo
alipofikia uamuzi huo wa kukifungia baada ya kujiridhisha kuwa kinaendeshwa
kinyume na utaratibu.
Waziri
Nape aliyefika uwanjani hapo saa 3:35 asubuhi,akiongozana na ujumbe wa wizara
na Mshauri Mkuu wa Mradi huo,Aloyce Mushi,alitaka kujua kwa undani zaidi
uhalali wa kiwanda hicho cha useremala,ambacho
kinakadiriwa kuwa na watumishi zaidi ya 15 kama kipo ndani ya mkataba wa ujenzi
wa Uwanja wa Taifa na eneo changamani la michezo.
Uwepo
wa kiwanja hicho kunapelekea ucheleweshwaji wa kukamilika kwa maboresho na
ujenzi wa Uwanja wa Uhuru.
Aidha
Waziri Nape amemuagiza Meneja wa Uwanja wa Taifa Rishe Urio kutoa maelezo ya
kina juu ya uwepo wa Kiwanda hicho katika eneo la ndani ya masaa 24 ni kwanini
akutoa taarifa juu ya uwepo wa shughuli za Kiwanda hicho katika eneo hilo ila
hali yeye ndiye msimamizi mkuu wa Uwanja huo.
Kwa
upande wake Meneja wa Kampuni ya BFG Cheng Longhai amekiri kuwa Kiwand hicho
kinaendeshwa kinyemela kwakuwa hakihusiani na mkataba wa kampuni hiyo.
Wakatihuohuo
Nape ameuagiza uongozi wa Selcom Tz kuhakikisha inakimilisha mfumo wa Tiketi za
Kielekroniki na kukabidhi kwa Serikali ndani ya siku 30 kuanzia sasa.
Agizo
hilo ni muendelezo wa kutekeleza maelekezo ya Mhe. Waziri Mkuu Kassim Majaliwa
Kassim wakati akiongea na wadau wa sekta ya michezo kwa mara ya kwanza toka
kuteuliwa kwake kuwa Waziri Mkuu.
Waziri
huyo anataraji kufanya ziara ya siku moja mkoani Shinyanga kesho,ambapo majira
ya saa nane mchana atakutana na waandishi wa Habari wa mkoa huo katika ukumbi
wa ofisi ya Mkuu wa Mkoa.